Wednesday, August 2, 2023

MGOGORO WAMALIZIKA MKANGE; WANANCHI WARIDHIA UJENZI WA BARABARA UENDELEE

Mkange, Chalinze


Mgogoro uliosababisha kusimama kwa utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Afrika ya Mashariki katika kata ya Mkange , umemalizika leo baada ya wananchi wa kata hiyo kukubali kupokea fidia na kupisha ujenzi wa barabara hiyo baada ya kukutana na Mbunge wa jimbo hilo la Chalinze Ndg . Ridhiwani Kikwete.


Mbunge huyo Ndg. Kikwete, ameeleza kufurahishwa kwake na kauli hiyo ya wananchi na amekielezea kitendo hicho kuwa cha kiungwana sana . Akieleza kwenye mkutano huo , Mbunge ameeleza kuwa maamuzi yaliyofikiwa ni wazi yanafungua sio tu milango ya maendeleo katika ukanda huu lakini pia ni ufunguzi mkubwa wa fursa za kukuza kiuchumi kwa wananchi hao.


Wakiongea katika nyakati tofauti, wananchi wa kata hiyo wamemshukuru Mbunge wao kwa kuingilia kati ili kulipatia ufumbuzi jambo Hilo lililodumu kwa muda mrefu. Pia wananchi hao walimshukuru Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia malipo hayo ya fidia.





 

No comments:

Post a Comment