Thursday, September 8, 2016

MATUKIO YA KIKAO CHA TATU BUNGENI MJINI DODOMA LEO TAREHE 08 SEPTEMBA 2016.

mbo1
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akisalimiana na Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzania na Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe (MB) wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.mbo2

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akijibu maswali ya wabunge wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.mbo3

Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzania na Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe (MB) akimuuliza swali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) kuhusu hali ya uchumi nchini ambapo Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa alimhakikishia kuwa Serikali ipo imara katika  kusimamia  ipasavyo uchumi wa nchi.mbo4

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akiwashukuru wabunge mara baada ya kumaliza kujibu maswali wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Leo Mjini Dodoma.mbo5
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na raia katika kuhakikisha inakabiliana na biashara haramu ya Madawa ya Kulevya.
 mbo7

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba akijibu swali bungeni ambapo alisema serikali ipo katika mazungumzo na serikali ya China kwa ajili ya kuboresha zao la Tumbaku.mbo8
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni akijibu swali bungeni ambapo alisema Wizara imetenga Shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuboresha hali ya Magereza nchini.mbo10

Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  akijibu swali bungeni ambapo alisema ambapo alisema Serikali imetenga shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuboresha Magereza ya watoto pamoja na makao ya Wazee nchini.mbo9

Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai akitoa mwongozo katika moja ya mambo wakati kikoa cha bunge kikiendelea mjini Dodoma.



No comments:

Post a Comment