Saturday, September 3, 2016

MIAKA 52 YA JWTZ, BAGAMOYO ILIKUWA HIVI.

Mkuu  wa Polisi wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP, Adam Maro, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, wakufunzi wa Mgambo Bagamoyo, pamoja na Mgambo kutoka kata mbalimbali za Bagamoyo, wakifurahipamoja kwa kuimba  nyimbo za gwaride mara baada ya kufanya usafi  siku ya tarehe 1 Septemba.


Sajenti Mwasimba, kutoka jeshi la nchi kavu makao makuu, akiwa amechuchumaa kwa mzuka wakati akiwaimbisha nyimbo mgambo wilayani Bagamoyo, katika maadhimisho ya miaka 52 ya  JWTZ.



Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ, Septemba mosi.



Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ.



Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga akihojiwa na waandishi wa  Habari huku akiwa juu  ya Trekta la  kubebea taka siku ya maadhimsho ya miaka 52 ya JWTZ Septemba mosi.
.....................................
Mwenyekiti wa kamati ulinzi na usalama wilaya ya Bagamoyo, majid Mwanga, amesema matukioya uhalifu wilayani humo  yamepungua ukilinganisa na kipindi cha nyuma.

Majid Mwanga ambae pia nia ni mkuu wawilaya ya Bagamoyo, alisema hali ya kupungua kwa uhalifu katika wilaya ya Bagamoyo, imetokana naushirikianouliopo katiyawananchi na vyombo vya ulinzina usalama ambapo raia wema wamekuwa wakitoa taarifa za kuwepo kwa wahalifu na kufanikisha kukamatwa.

Hayo aliyasema wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania siku iliyoadhimishwa kwa kwa kufanya usafi ambapo kwa Bagamoyo Jeshi la akiba (Mgambo) lilitumika kutekeleza usafi huo huku mkuu wa wilaya akishiriki kwa kuendesha Trekta la kubebea taka kuanzia asubui mpaka jioni.

Aidha, aliwataka wananchi  wilayani humo kuwa wazalando kwa kuipenda nchi yao na kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani ambavyo vitakavyopelekea serikali kutumia nguvu kukabiliana navyo na kusababisha hasara  kwa taifa mahusiano mabaya kati ya wananchi na serikali yao.

Alisema, wanaofanya vitendo vya uvunjifu  wa  amanai siku  zote  ni  watu  wachache, serikali  inapotumia  nguvu kupambana nao  wataathirika na  wananchi wasiokuwa  na hatia jambo ambalo linaweza kuleta uhasama miongoni mwa  vikosi vya ulinzi na usalama.
 Diwani, wa kata ya Kiromo Mh. Hassani R. Usinga. (Wembe).

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Kiromo, Hassani Usinga (Wembe) aliwataka mgambo kuwa wazalendo ili serikali ifaidike nakuwepo kwajeshi  hilo  la akiba, kwa kushiriki katika matukiombalimbali pale wanapohitajika.
Alisema sivyema kumuona mgamboanaitwa akatekeleze majukumu yake halafu anakwepa jambo  ambalo halitakiwi kwa mgambo aliyekula kiapo  cha utii na uwajibikaji katika shughuli za kitaifa.

Aliongeza kuwa, mgambo ni  jeshi la akiba ambaloserikali za kata zinawategemea kuimarisha ulinzi katika kata zao hivyo wakinesha nidhamu na uwajibikaji serikali za kata zinaweza kuwajengea vituovitakavyotoa huduma ya ulinzai kwa jamii.

Alisema tayari yeye katika kata ya Kiromo ameandaa mpango wa kujenga kituo ambapo mgambo watakaa hapo ili kurahisisha shughuli za ulinzi na usalama.

Akizungumzia hali ya usafi  katika mji wa Bagamoyo mkuu huyo wa wilaya aliwataka wananchi kudumsha usafi ili kuepuka magonjwa mbalimbali ya kuambukiza, na kusisitiza kuwa usafi wa pamoja katika mji wa  Bagamoyo  utafanyika mara mbili kwa mwezi.

Kufuatia mkakati huo wa kufanya usafi wa pamoja mara mbili kwa mwezi, mkuu huyo wa wilaya aliwaagiza mgambo kuwakamata watu wote watakaofungua biashara zao katika siku zilizotangazwa kufanya usafi.

Aidha, alimuagiza Afisa mazingira wilaya ya Bagamoyo,kuwachukulia hatua wafanyabiashara wote ambao hawajaweka vifaa vya kutupia taka kwenye maeneo yao ya kufanyia biashara vinginevyo atamuwajibisha yeye.


Mkuu  wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga akiwa na katibu tawala wa wilaya, Erica Lyegela wakipita mitaani kukusanya taka  na  Trekata na kwenda  kuzimwaga Dampo, katiKa maadhimisho  ya miaka 52 ya JWTZ. Septemba mosi.


Mkuu  wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga akiwa na katibu tawala wa wilaya, Erica Lyegela wakipita mitaani kukusanya taka  na  Trekata na kwenda  kuzimwaga Dampo, katiKa maadhimisho  ya miaka 52 ya JWTZ. Septemba mosi.



Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo, ambae  piya ni Mwenyekiti wa  kamati ya  ulinzi  na usalama wilaya, Majid Mwanga mwenye miwani  kushoto akipiga kwata  pamoja na  mgambo na  kwanja lake begani, ilikuwa  ni siku ya  maadhimisho ya miaka 52 ya JWTZ, Septemba mosi.

Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo, ambae  piya ni Mwenyekiti wa  kamati ya  ulinzi  na usalama wilaya, Majid Mwanga mwenye miwani  kushoto akipiga kwata  pamoja na  mgambo na  kwanja lake begani, ilikuwa  ni siku ya  maadhimisho ya miaka 52 ya JWTZ, Septemba mosi.
Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo, ambae  piya ni Mwenyekiti wa  kamati ya  ulinzi  na usalama wilaya, Majid Mwanga mwenye miwani  kushoto akipiga kwata  pamoja na  mgambo na  kwanja lake begani, ilikuwa  ni siku ya  maadhimisho ya miaka 52 ya JWTZ, Septemba mosi.


Mwenyekiti wa  kamati  ya ulinzi na  Usalama wilaya, Mkuu  wa  wilaya ya  Bagamoyo Majid Mwanga, kulia, pamoja nae mkuu wa polisi wilaya ya Bagamoyo, mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP-Adam Maro wakiimba na kucheza pamoja na mgambo siku ya maadhimisho ya miaka 52 ya JWTZ, Septemba mosi.



Ni siku ya sherehe baada ya usafi viongozi walishiriki na mgambo kuimba nyimbo na kucheza pamoja, Klia ni Mwenyekiti wa  kamati ya ulinzi na Usalama wilaya, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid mwanga, wa tatu  kulia mwenye sare za polisi ni mkuu wa Polisi wilaya ya bagamoyo, mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam Maro kwa mbali anaonekana Afisa tarafa wa Yombo Mzee Kidelenya, Kushoto ni katibutawala wa wilaya ya Bagamoyo, Bi, Erica Lyegela wakiongozwa kwa nyimbo  na Mkufunzi wa  Mgambo kutoka Jeshi la  nchi kavu makao makuu ya jeshi, Sajenti Mwasimba, ambae yupo mbele yao.

Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ, Septemba mosi.
Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ, Septemba mosi.
Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ, Septemba mosi.
Mgambo wilayani Bagamoyo, wakiwa imara kupokea maelekezo kutoka kwa wakufunzi  wao, wakiwa wamebeba mafagio Reki, na Kwanja, kwaajili ya usafi siku ya  maadhimisho  ya  miaka 52 ya  JWTZ, Septemba mosi.



Mgambo wakiendelea na usafi katika mitaa ya Bagamoyo wakati wa maadhimisho wa ya miaka 52 ya JWTZ.



Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo majid Mwanga akibinua tera la  taka, eneo la kutupia  taka.



Mgambo wakirejea ofisi ya mkuu wa wilaya mara baada ya kumaliza kufanya usafi.



Mgambo wakiwa wamewasili ofisi ya mkuu wa wilaya wakiongozwa na Mkufunzi wao kutoka jeshi  la nchi kavu kutoka makao makuu ya  jeshi Sajenti Mwasimba.



Mkuu wa Polisi wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam Maro, akiwa anasisitiza jambo wakati akizungumza na mgambo katika Ofisi ya mkuu wa  wilaya.


Katibu tawala wilaya ya Bagamoyo, Erica Lyegela, akiangalia  mazingira ya  usafi katika  ofisi  ya  mkuu wa wilaya.

Mkuu  wa  wilaya ya  Bagamoyo,  Majid Mwanga akisisitiza  kwamba  usafi pamoja Bagamoyo  ni  siku 2  kwa  mwezi.

No comments:

Post a Comment