Thursday, September 29, 2016

DC. BAGAMOYO AWAKUTANISHA WAFUGAJI NA WAKULIMA KUJADILI MIGOGORO BAINA YAO.


Wafugaji na wakulima wakiwa kwenye mkutano wa pamoja ulioitishwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid hemed mwanga.
Meza kuu, Kutoka kushoto mkurugenzi Halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa, wa  pili kushoto ni mwenyekiti wa kikao hicho mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed  Mwanga, wa tatu kutoka kushoto ni Mbunge wa jimbo  la Bagamoyo Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, na wa kwanza kulia ni kaimu mkurugenzi  Halmashauri ya Bagamoyo, Dkt. Amiri Batenga. 
..........................


Mkutano huo umeitishwa ili kujadili migogoro baina yao, mkutano huo uliofanyika katika ukumbi  wa chuo cha uongozi wa elimu Bagamoyo (ADEM) umewajumuisha wenyeviti wa vijiji wote, watendaji kata wote, maafisa tarafa wote, maafisa kilimo na mifugo wa kata zote zawilaya ya Bagamoyo  pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya.

Lengo la kikao hicho ni  kutafuta ufumbuzi wa  migogoro inayotokea mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji ambapo hivi  kari buni kumeripotiwa matukio ya mapigan na  kutishiana amani b aina ya  pande hizo mbili.

Migogoro hiyo pamoja na madhara mbalimbali yaliyotokea  ikiwemo  wakulima kukimbia mashamba yao,  wafugaji nao  kupoteza mifugo yao pia imepelekea kuuwawa kwa mfugaji katika kata ya Makurunge, na mama mmoja mkulima kuuwawa kwa  kukatwa  katwa na mapanga na hatimae kumtia ndani ya  shimo  la  choo huko kata ya  miono.

Kufuatia hali hiyo ilimulazimu  mwenyekiti wa kamati ya  ulinzi na usalama wilaya ya Bagamoyo ambae ndiye mkuu  wa wilaya kuitisha  kikao cha  pamoja ili  kutafuta  ufumbuzi.

Katika kikao hicho kilichodumu  kwa muda wa saa 10 kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 1 usiku,  kilitoka na maazimo 18 ambayo yanahitajika kutekelezwa ili kuepuka migogoro hiyo isijirudie.

Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendelea katika kikao hicho


Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendelea katika kikao hicho

Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendele katika kikao hicho

 Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendele katika kikao hicho



Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Bagamoyo ikifuatilia yanayoendelea katikakikao hicho


Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Bagamoyo ikifuatilia yanayoendelea katikakikao hicho


Mtaalamu kutoka idara ya Ardhi Mosesi Kibona akitoa elimu juu matumizi bora ya Ardhi katika kikao hicho

Wataalamu  kutoka Halmashauri ya Bagamoyo wakifuatilia kwa makini yanayoendelea katika  kikao hicho, wa kwanza kulia ni  Mchumi- idara ya Mipango Halmashauri ya Bagamoyo, Jalala Samata na watatu kutoka kulia ni Afisa Mifugo kutoka idara ya Mifugo Bagamoyo, Sinani R. Simba.

Mwenyekiti wa chama cha wafugaji mkoa wa Pwani, Mohamedi Geboe akielezea  changamoto wanazokumbana nazo wafugaji.

 Afisa Mifugo kutoka idara ya Mifugo Bagamoyo, Sinani R. Simba, akifafanua sheria ya mipango miji kuhusu mifugo

Katibu tawala wa wilaya ya Bagamoyo, Erica Lyegela akitoa muongozo wa  kikao hicho

 Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendelea katika kikao hicho


Mwenyekiti wa mkutano huo, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemedi Mwanga akisikiliza kwa makini hoja na maoni ya pande zote katika kikao hicho ambacho  kimelenga  kumaliza migogoro ya wakulima na  wafugaji wilayani Bagamoyo.

Mkuu wa Polisi wilaya ya kipolisi Chalinze, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Janeth Magomi,  akielezea idadi ya kesi, kati ya wakulima na wafugaji zilizoripotiwa polisi katika Halmashauri ya Chalinze.

Mkuu wa Polisi wilaya ya kipolisi Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam A. Maro, akielezea idadi ya kesi kati ya wakulima na wafugaji zilizoripotiwa polisi katika Halmashauri ya Bagamoyo.

 Wakulima na wafugaji wakifuatilia yanayoendele katika kikao hicho
Maafisa tarafa wakifuatilia kwa makini yanayoendelea katika kikao hicho.

Maafisa tarafa wakifuatilia kwa makini yanayoendelea katika kikao hicho.



No comments:

Post a Comment