Thursday, September 22, 2016

TAARIFA YA RC. MAKONDA KUHUSU KAMPENI YA AFYA CHEKI

kod1
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari LEO jijini Dar es Salaam kuhusu kampeni ya kupima afya bure ambayo inaratibiwa na ofisi yake kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Hospitali za rufaa za Mkoa wa Dar es Salaam na Afya Check ya Clouds FM pamoja na wadau wengine. Kampeni ya kupima afya itafanyika Septemba 24 na 25, mwaka huu kwenye viwanja vya Mnazi mmoja siku ya Jumamosi na Jumapili.
..................................


TAARIFA  YA MKUU WA MKOA MH. PAUL MAKONDA
Napenda nichukue fursa hii kuwajulisha kuwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam imeandaa zoezi la kiafya kwa wananchi wote wa Mkoa wa Dar es Salaam linalotarajia kufanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 24/09/2016 siku ya Jumamosi na tarehe 25/09/2016 siku ya Jumapili kuanzia saa mbili kamili asubuhi katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Ndugu Wananchi,
Napenda kuwajulisha kuwa hii ni habari njema kwetu kwani huduma zote za vipimo zitatolewa bure bila gharama yoyote hivyo tunaombwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hili la kuzijua vema afya zetu kwani itatuwezesha kijikinga na magonjwa yanayoweza kijitokeza, kuepuka matumizi ya gharama kubwa za matibabu, na kuzuia vifo visivyo vya lazima kwani kuna wengine huenda hospitali pindi hali imekua mbaya sana.

Ndugu Wananchi,
Napenda kuwajulisha kuwa KILA AINA YA UGONJWA KATIKA MAGONJWA KUMI MAKUBWA kama vile Shinikizo la Damu, Kisukari, Saratani ya Matiti, Saratani ya Shingo ya Uzazi, Tezi Dume, Saratani ya ngozi kwa albino na Magonjwa mengine mengi yatapimwa.
Hivyo wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam mnahamasishwa kufika kwa wingi kwani MADAKTARI BINGWA kutoka HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI, TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD, TAASISI YA MOYO YA JAKAYA MRISHO KIKWETE, HOSPITALI ZA RUFAA ZA MKOA WA DAR ES SALAAM, HOSPITALI YA AGAKHAN, TAASISI ZA CCP MEDICENE wote kwa pamoja watakuwa tayari kuwahudumia.

Ndugu Wananchi,
Ninaimani ya kuwa kila mmoja wetu anajua umuhimbu wa AFYA YAKE kwani utakapoijua vema afya yako itakusaidia kuwa salama kila iitwapo leo na kukupelekea kuwa na nguvu ya kufanya kazi kwa bidii ili kujipatia kipato cha kila siku sambamba na kuinua uchumi wa Taifa letu la Tanzania.

CHEKI AFYA YAKO KWA UBORA WA MAISHA YAKO
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA

Paul C. Makonda
MKUU WA MKOA WA
DAR ES SALAAM
 kod2

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Onesmo Kisanga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) LEO akizungumzia kuhusu umuhimu wa kupima afya mara kwa mara ili kuzuia uwezekano wa mtu kupata matatizo makubwa ya magonjwa ya figo.
 kod3

Baadhi ya waandishi wa habari na madaktari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati akiwahamasisha wananchi wa Jiji la Dar es Salaam na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kupima afya Septemba 24 na 25, mwaka huu.
 kod4

Kutoka kushoto ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ilala, Victoria Ludovick, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Onesmo Kisanga wa Muhimbili na Mshauri Mtaalamu wa Uchunguzi wa Magonjwa ya Figo, Dk Omar Sherman wa Hospitali ya Aga Khan wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda LEO.
 kod5

Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk Praxeda Ogweo amewataka wananchi kujenga tabia ya kupima afya hasa kina mama kupima endapo wanaviashiria vya kansa au la.
 kod6

Mganga Mkuu wa Kinondoni, Dk Aziz Msuya akizungumza katika mkutano wa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika kampeni ya kupima afya ambayo itafanyika Septemba 24 na 25, mwaka huu. 
 kod7

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa afya wa jijini Dar es Salaam Leo. Kutoka kulia ni Mshauri Mtaalamu wa Uchunguzi wa Magonjwa ya Figo, Dk Omar Sherman wa Hospitali ya Aga Khan, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Onesmo Kisanga wa Muhimbili, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Muhimbili, Dk Hedwiga Swai, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali Muhimbili, Dk Juma Mfinanga na Mganga Mkuu wa Kinondoni,  Dk Aziz Msuya.

No comments:

Post a Comment