Monday, September 5, 2016

UJUIO WA MUFTI MENKI, AREF NAHDI, AISHUKURU SERIKALI KWA USHIRIKIANO. MUFTI MENKI AWAASA WAISLAMU KUISHI DUNIANI KAMA WAPO SHULE.

 
Mwenyekiti wa The Islamic Foundatio, Aref Nahdi, kulia akiwa na Muft Ismail Menk wa Zimbabwe
Mwenyekiti  wa The  Islamic Foundation Aref  Nahd 
 
Mufti, Ismaili Menki wa Zimbabwe
............................................................

Waislamu wametakiwa kuishi  katika dunia kama wapo shuleni ili kutekeleza  malengo  maalum ya kuumbwa kwa binadamu hapa duniani.

Wito huo umetolewa  jijini Dar  es Salaam, na Mufti wa Zimbabwe Sheikh, Dkt. Ismail  Menk, alipokuwa akitoa  hutuba  katika  ukumbi wa  Diamond Jublee ambapo amewataka waislamu kutambua kwamba yapo maisha mengine baada ya  kufa.

Alisema mtu anapokufa ataulizwa kuhusu  maisha yake ya duniani,hivyo inampasa  kila  muislamu kuchukua tahadhari katika  maisha yake ya kila siku.
Mufti Menki aliongeza  kuwa ili  kupata  mafanikio duniani na akhera,muislamu anapaswa kusihi kwa kutekeleza sheria za  mwenyeziMungu bila ya kuchagua ikiwa ni pamoja na kuwa mahusiano mema miongoni mwa jamii ili kuweza kuonyesha uzuri wa  uislamu.

Alisema  muislamu hapaswi kudharau dhambi yoyote kwa  kufikiri  kwake  kwamba dhambi fulaninindogo kwani  kila analofanywa linaandikwa  na kutolea mfano  wa  mwanaume anyemtazama  mwanamkebarabarani na kumsifia maumbile yake ja mbo  ambalo ni makosa kwakuwa amriimekuja ya kuinamisha  macho ili usiangalie  vilivyoharamishwa kwako.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa The Isalamic Foudation yenye makao yake makuu mjini morogoro Nchini Tanzania, Al akhi, Aref Nahdi, alisema ujio wa Mufti Menki hapa Tanzania  umefungua milangoyamahusiano mema  miongoni mwa waislamu katika Afrika jambo  am balo linapaswa kuenzia kwa namna yoyote.

Aref  amesema ili kuthamini mchango wa  Mufti Menki, Taasisi ya The Islamic Foundation itaandaa mualiko maalum kwa ma mufti kutoka Afrika ili waje Tanzania ambapo watafanyamkutano pamoja na mufti wa tanzania lengolikiwa ni kuinyoshe jamii umoja namshikamano uliopo miongoni mwa waislamu.

Alisema  mkutano huo utatoa fursa kwa viongozi hao wa kiislamu  barani Afrika ambao wana hadhi ya Umufti, (Maprofesa) kubadilishana mawazo na kuangalia njia sahihi za kufikisha  ujumbe  ili jamii ijue kwamba  uislamu sio dini ya vurugu na badala yake kila anaetaka amani anapaswa  kuchukua  mfano kutoka  kwenye uislamu.

Aidha, Mwenyekiti huyo wa The  Islamic Foundation Tanzania, Aref Nahdi ambae ndie mwenyeji wa Mufti Menki, alisema anatoa shukrani kwa serikali ya tanzania  kwa kuthamini ujio  wa Mufti Menki, hali iliyopelekea wepesi wa kusafiri  kati ya Dar es salaam na  Morogoro.

Ameimba serikali iendelee kutoa ushirikiano kama huo mara  wageni wa kiislamu wanapoingia hapa nchini  kwani  katikakujenga mahusiano mema kati ya nchi na nchi  ni  pamoja mapokezi mazuri ya kiserikali kwa wadini kutoka nje ya nchi ambapo taasisi The Islamic Foundation  i mepanga kuwaleta  viongozi kadhaa wa kiislamu hapa nchini ambapo pamoja na kulingania  katika uislamu, viongozi hao wa kigeni pia  watapata fursa ya kuchangia katika huduma  za jamii hapa  nchini ikiwemo huduma  za Afya,  Elimu  pamoja na maji.        
 

Mwenyekiti wa The Islamic Foundation Aref Nahdi akiwa na Mufti  Menki  na  wajumbe  waandamiz.

                                               
Mufti Ismail Menki, wa  Zimbabwe akisaini kitabu cha  wageni mara   baada ya kuwasili  katika ofisi za  The  Islamic  Foundation Mjini Morogoro  nchini Tanzania, Kulia  ni  Mwenyeji  wake,  Mwenyekiti wa  The Islamic Foundation, Aref Nahdi
                                                                            
Waislamu wakimsikiliza Mufti Menki, katika ukumbi wa Diamond jublee, jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa  akihutubia.
                                                                                                                                                                                                                                                                                                       
                                                                                                                                                                                                                                                                   

No comments:

Post a Comment