Sunday, September 18, 2016

MHALIFU SUGU NA MBAKAJI AUWAWA KIBAHA

rpc-pwani
 Kamanda wa Polisi  mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi wa Polisi ACP-Bonaventura Mushongi wa kwanza kushoto.
.........................................................

 Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MICHAEL William maarufu Michael dada ambae alikuwa akidaiwa ni mhalifu sugu na mbakaji huko wilayani Kibaha ameuwawa na wananchi wenye hasira kali.

Michael ameuwawa huko kwenye pori la shirika la elimu Kibaha-Tumbi,akidaiwa kuwateka watoto wa kike wawili ambao ni wanafunzi kwa lengo la kuwabaka.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani,Bonaventura Mushongi akizungumzia tukio hilo,alisema watu hao walimshambulia mtu huyo sehemu mbalimbali za mwili na kumsababishia kifo.

Kwa mujibu wa kamanda huyo wa polisi,alisema tukio lilitokea juzi saa 10 alasiri.

Alisema marehemu huyo alimchukua mwanafunzi mwenye umri wa miaka (11) anaesoma shule ya msingi Kibaha na mwingine mwenye miaka (6) mwanafunzi wa shule ya chekechea ya mama Kawili wote wanaishi Picha ya Ndege.

Watoto hao walikuwa wakicheza rede mtaani kwao karibu na baa ya Lekashingo kata ya Picha ya Ndege ambapo Michael aliwashawishi wamsindikize mtaa wa Lulanzi kwenda kuchukua mzigo wake ambao aliusahau”
“Watoto hao walimkubalia na kuanza kuongozana nae lakini wakiwa njiani ghafla lilitokea gari aina ya toyota noah nyeusi ambayo haikuweza kufahamika namba zake za usajili na kuondoka nao kwenda nao pori la shirika la slimu Kibaha karibu na shule ya sekondari ya Tumbi’
“Wakiwa katika pori hilo mtoto mkubwa alimponyoka wakiwa wamefika kwenye bwawa la maji machafu kisha kuomba msaada ndipo kundi la watu lilipojitokeza na kuanza kumkimbiza na walipomkamata walimpiga hadi kufariki dunia,” alisema kamanda Mushongi.

Kamanda Mushongi ,alisema uchunguzi uliofanywa na jeshi la polisi umebaini marehemu alikuwa mhalifu mzoefu na alikuwa akifanya matukio ya mara kwa mara ikiwemo ya ubakaji na wizi wa mifugo.

Alisema hivi karibuni alikamatwa na kufikishwa mahakama ya wilaya ya Kibaha kwa kosa la kuiba ngombe wanne.

Michael aliachiwa huru yeye na mwenzake Said Mohamed baada ya mlalamikaji kushindwa kufika mahakamani baada ya kuwapata ngombe wake kwa kesi iliyofunguliwa namba KBH/STPU/02/2014.

Jeshi hilo limewakemea wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi badala yake wawafikishe watuhumiwa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.

No comments:

Post a Comment