Thursday, September 22, 2016

HOSPITALI YA KISASA IMEJENGWA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI (MUHAS) ENEO LA MLONGANZILA JIJINI DAR ES SALAAM.

mlo4
Muonekano wa Hospitali ya Kisasa ya kufundishia wataalamu wa Afya na kutoa huduma ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)   iliyopo eneo  la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Hospitali hiyo hiyo ya kisasa inatarajiwa kufunguliwa rasmi Januari Mwakani.
 mlo1

Daktari Bingwa  wa Uchunguzi wa mionzi kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dr Lulu Fundikira akiwaonyesha waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali  mashine ya CT-Scan iliyopo kwenye Hospitali ya Kisasa ya kufundishia wataalamu wa Afya na kutoa huduma iliyopo eneo  la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati waandishi hao walipotembelea hospitali hiyo jana. Hospitali hiyo hiyo ya kisasa inatarajiwa kufunguliwa rasmi Januari Mwakani.
 mlo2

Daktari Bingwa  Wa tiba za dharura kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dr Andrew Sawe akiwaonyesha waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali  vitanda vya kisasa kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu viliyopo kwenye Hospitali ya Kisasa ya kufundishia wataalamu wa Afya na kutoa huduma iliyopo eneo  la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati waandishi hao walipotembelea hospitali hiyo jana. Hospitali hiyo hiyo ya kisasa inatarajiwa kufunguliwa rasmi Januari Mwakani.
....................................


Hospitali ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) , iliyojengwa kisasa kwa kutumia mifumo mbalimbali ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA, itakuwa ya kwanza kutumia mfumo wa teknolojia ya sampuli hewa, unaochukua vipimo kwa mtambo maalum na kuwasilisha majibu kwa njia ya mtandao.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ziara maalum katika jengo hilo lililokamilika ujenzi wake rasmi tangu Agosti, mwaka huu, Makamu Mkuu wa chuo cha MUHAS, Profesa Ephata Kaaya, alisema hospitali hiyo, itatoa tiba ya magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa sugu kama vile, moyo, saratani na figo.

Hospitali hii ni  ya kisasa ya kufundishia wataalamu wa afya na kutoa huduma ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) iliyopo eneo la kampasi ya Mloganzila jijini Dar es Salaam, inatarajiwa kufunguliwa  na kuanza kutoa huduma Januari mwakani.

Hospitali hiyo, imejengwa na kufungwa vifaa tiba vya kisasa vya digitali, vinavyotumia zaidi teknolojia ya Tehama zikiwemo mashine za X-ray, MRI, CT-Scan, mashine maalum kwa ajili ya kupimia magonjwa ya wanawake, mashine maalum za kupima na kutibu meno, koo, masikio na pua.

“Pia umefungwa mtambo wa kisasa zaidi wa sampuli hewa uliopo katika kila idara na kuunganishwa na maabara ambao kazi yake ni kusafirisha vipimo na kupeleka sehemu mbalimbali na majibu ya vipimo hivyo huwasilishwa sehemu husika kwa njia ya mtandao,” alisema.

Alisema mtambo huo, unasaidia kupunguza tatizo la msongamano katika chumba cha maabara, unaongeza ufanisi na usahihi wa vipimo lakini pia hupunguza muda na kuepusha mkanganyiko wa vipimo.

 Hospitali hiyo pia itatoa huduma za kufundishia, kufanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali na tafiti za fani za afya. “Lakini pia tuna vyumba maalum 12 kwa ajili ya wagonjwa wenye magonjwa ambukizi kama vile ebola, kipindupindu na kifua kikuu.

Profesa Kaaya, amesema ujenzi wa hospitali hiyo uliogharimu kiasi cha dola za Marekani milioni 94.5 katika eneo hilo la Mloganzila lenye ukubwa wa ekari 3,800, ulianza tangu mwaka 2014 kupitia mkopo wenye riba nafuu ambao malipo yake yataanza kulipwa baada ya miaka 15 kwa kipindi cha miaka 25.

Amesema jengo la hospitali hiyo lina ghorofa tisa ambazo zinajumuisha vyumba 13 vya upasuaji kikiwemo chumba kimoja cha upasuaji kwa wagonjwa wa dharura, wodi za watoto, maabara za kisasa, vyumba vya wagonjwa mahtuti na kusafisha figo, wodi za kujifungulia, chumba cha kuhifadhia maiti na vyumba vya kufundishia.

Aidha amesema katika eneo la wodi zipo wodi 12 za wagonjwa mashuhuri vikiwemo vyumba viwili vyemye mitambo ya kisasa ya kufuatilia hali ya mgonjwa vya viongozi wenye hadhi ya juu ikiwemo Rais.
 mlo3

Daktari Bingwa  wa koo, Masikio na Pua kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dr Daudi Ntunaguzi akiwaonyesha waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali  utendaji kazi wa moja ya kifaa cha kisasa cha kuchunguza masikio kilichopo  kwenye Hospitali ya Kisasa ya kufundishia wataalamu wa Afya na kutoa huduma iliyopo eneo  la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati waandishi hao walipotembelea hospitali hiyo jana. Hospitali hiyo hiyo ya kisasa inatarajiwa kufunguliwa rasmi Januari Mwakani.
 1

Baadhi ya madaktari bingwa na wataalamu mbalimbali wakisikiliza maelezo ya wataalamu wa ujenzi wa jengo hilo yaliyowasilishwa leo mbele ya waandishi wa habari.


 2

Juma Bernard Mkuu wa Kitengo cha Mfumo wa Mawasiliano MUHAS Academic Medacal Centre Mloganzila akifafanua jambo katika maelezo kwa waandishi wa habari wakati alipotembelea hospitali hiyo.
 3

Profesa Ephata  Kaaya akizungumza na waandishi wa habari na kuwaelezea juu ya mradi wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS   iliyopo eneo  la Mloganzila nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam , Kulia ni Makamu Mkuu wa chuo hicho Profesa Said Aboud.
 4

Omari Kileo Mhandisi wa Umeme MUHAS Academic Medacal Centre Mloganzila  akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati alipotembelea na kujionea ujenzi wa  chuo hicho.
 6

Andrew Fungamali akielezea jinsi mfumoa wa  maji safi na maji taka unavyofanya kazi katika chuo hicho.
 7

Andrew Fungamali akielezea na kuonyesha jiko kwa ajili ya kupikia chakula cha wagonjwa katika chuo hicho.


No comments:

Post a Comment