Sunday, September 11, 2016

TETEMEKO LA ARDHI KAGERA, WATU 11 WAFARIKI NA WENGINE KADHAA KUJERUHIWA, NYUMBA ZABOMOKA

4
Mkuu wa wilaya ya Bukoba Mh. Deodatus Kinawiro amethibitisha kufariki kwa watu 11 na wengine 196 kujeruhiwa  katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kufuatia tetememko la ardhi lenye ukubwa wa vipimo vya 5.7 lililotokea  mkoani humo na kusababisha madhara makubwa.

  Alisema tetemeko lililotokea mchana wa jana jumamosi tarehe 10 septemba 2016 lilikuwa ni kubwa na limeathiri majengo mengi na kusababisha majeruhi na vifo.

Hata hivyo bado Kamati ya Ulinzi na Usalama ikishirikiana na vikosi vya uokoaji pamoja na majeshi la ulinzi na usalama vinaendelea kufanya tathmini ya uharibifu wa majengo na mali uliosababishwa na  Tetemeko hilo.

DC Kinawiro ameongeza kwamba taarifa zaidi zitaendeleo kutolewa kadri zitakavyopatikana  kutokana na kuendelea kwa kazi ya  tathmini ya athari ya tetemeko hilo.

No comments:

Post a Comment