Thursday, October 6, 2016

MUWEKEZAJI ATOA MSAADA WA GARI ZAHATI YA MIHUGA BAGAMOYO.

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akionesha funguo ya gari iliyotolewa msaada na muwekezaji, Abdallaah Sadi kwaajili ya kubebea wagonjwa katika Zahanati ya Mihuga, wanaoshuhudia kulia nimkuu wa wilaya ya Bagamoyo,  na kushoto ni mjumbe  wa kamati ya  siasa kata ya Kiwangwa, Amiri Mkang'ata.


Katikati ni muwekezaji wa aliyetoa Gari hilo Abdallaah Sadi, kulia ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majidi Mwanga na kushoto ni  mbunge wa jimbo  la Chalinze Ridhiwani  Kikwete ambapo nyuma yao ni Gari aina aina ya TOYOTA NOAH lililotolewa na muwekezaji  huyo kwaajili ya zahanati ya Mihuga.



Wananchi wa kijiji cha Mihuga wakishuhudia makabidhiano yaGari hilo.



Mbunge wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Kikwete akizungumza mara baada  kukabidhiwa Gari hilo



Muonekano wa Gari iliyotolewa msaada kwa Zahanati ya Mihuga iliyopo kata ya Miono wilayani Bagamoyo.



Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akijaribu  gari hilo




Daktari wa zahanati ya Mihuga Grace Mitumba akijaribu Gari hilo lililotolewa  kwaajili ya Zahanati hiyo ilyopo kata ya Miono, aliyekaa kiti cha nyuma ni Mbunge wa jimbo la Chaline Ridhiwani  Kikwete

No comments:

Post a Comment