Thursday, October 6, 2016

MWALIMU WA MADRASA BAGAMOYO ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUENDESHA MAFUNZO YA KIHALIFU KWA WATOTO.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi wa Polisi, ACP- Boniventure Mushongi.
......................................................

Jeshi  la Polisi mkoani  Pwani linamshikila mwalimu wa madrasa  kwa tuhuma za kuendesha  mafunzo ya  kihalifu katika madrasa yake.

Akitoa Taarifa kwa vyombo vya Habari kamanda wa Polisi Mkoawa Pwani, Kamishna msaidizi wa Polisi, ACP-Boniveture Mushongi alisema mwalimu huyo amekamatwa kutoka  na taarifa walizopata kutoka raia wema ambao walikuwa na mashaka kuhusu mwenendo wake.

Kamanda Mushongi alisema mwalimu huyo mwanamke  Ashura Saidi mwenye umri wa miaka 47, ni mwalimu wa  madrsa  ijulikanayo kwa jina la ARAHMA, iliyopo eneo la Kimarang'ombe kata ya Nianjema Tarafa ya Mwambao wilayani Bagamoyo alikamatwa kufuatia msako wa kushtukiza  uliofanywa na makachero majira ya saa 9 za jioni siku ya tarehe 01 Oktoba  2016.

Kamanda Mushongi aliongeza kuwa katika upekuzi mtuhumiwa  alikutwa na bomu  la moshi lenye namba G2020c.SS-ATCS lililokutwa kwenye makazi yake.

Aliongeza kuwa katika uchunguzi wa awali umebaini madrasa hiyo inamilikiwa na taasisi ya AKHA LAAGUL ISLAM ambayo ilisajiliwa kwa lengo la  kulelea watoto yatima.

Kituo hicho kimekuwa kikitoa huduma kwa watoto kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo Dar es Salaam, Handeni Tanga, Mlandizi, na Bagamoyo mkoani Pwani.

Aidha, Kamanda Mushongi  alisema kuwa  pamoja na kumshikilia mwalimu huyo wa Madrasa, polisi inawashikilia watoto 22 waliokuwa katika kituo hicho am bao 16 kati yao ni wasichana na 6 ni wavulana.

No comments:

Post a Comment