Saturday, October 29, 2016

WADAU WA ELIMU KUTOKA CHUO KIKUU CHA SAYANSI UJERUMANI WATEMBELEA SHULE YA MSINGI MWASAMA BAGAMOYO


Kushoto ni  Mkurugenzi wa shule ya msingi MWASAMA iliyopo Bagamoyo, Mwajuma Saidi Masaiganah akiwa na wageni wake mara walipotembelea katika shule ya MWASAMA, kulia ni Agnes Weber na katikati ni Bernd Sdiapers.
Mkurugenzi wa shule ya msingi  MWASAMA, Mwajuma Saidi Masaiganah akiwa na wageni wakeofisini kwake mara walipowasili shuleni hapo kujionea maendeleo ya shule hiyo.
..........................................


Wadau wa elimu kutoka chuo kikuu cha sayansi cha Ujerumani, wametembelea shule ya msingi ya  MWASAMA iliyopo Bagamoyo ili kuona mafanikio yanayopatikana katika shule hiyo.

 Akizungumza mara baada ya kuwapokea wageni hao, mkurugenzi wa shule ya MWASAMA,  Mwajuma Saidi Masaiganah alisema anawasukuru wadau hao wa elimu  kwa kufika katika shule hiyo ili kubadilishana uzoefu na michango mbalimbali katika maendeleo ya elimu.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kutoa shukrani zake kwa wadau hao ambao waliweza kufadhili ujenzi wa madarasa mawili, Vitabu vya sayansi, pamoja na umeme wa sola ikiwa kama mchango wao kwa shule hiyo.

Mkurugenzi huyo washule ya MWASAMA alisema kuwa wadau hao wa elimu  licha ya kutoa msaada huo katika shule hiyo pia wameweza kutoa msaada wa vitabu katika shule mbalimbali hapa nchini wakiwa na lengo kuonyesha namna wanavyothamini sekta ya elimu.

Mwajuma aliwaeleza wageni hao kuwa licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo, wamefanikiwa kushika nafasi ya 1 wilaya kati ya shule 13 zilizopo kwenye kundi hilo, nafasi ya 1 mkoa kati ya shule 323 katika matokeo ya mtihani wa darasa  la saba  2016 huku kitaifa ikishika nafasi ya 33 kati ya shule 8241.

Alisema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na ushirikiano na wadau mbalimbali wa  elimu wakiwemo wao ambao wameweza kusadia kutatua baadhi ya changamoto shuleni hapo.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mhadhiri wa chuo kikuu cha Sayansi kutoka ujerumani,Bernd Sdiapers alisema ujio wao katikashule hiyo umetokana na namna uendeshaji wa shule hiyo unavyozingatia thamani ya kumpa mtoto elimu.

Alisema ili jamii iweze kutekeleza mambo mbalimbali ya kimaendeleo inahitaji kuwa na  elimu, hivyo kitendo cha kuwapa watoto elimu  kinahitaji kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa elimu ili kuwa na jamii yenye wataalamu wa fani mbalimbali.

Aidha, aliipongeza shule ya MWASAMA kwa kushika nafasi ya kwanza wilaya ya Bagamoyo, katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2016.

Alisema hiyo ni kazi nzuri in ayofanywa na mkurugenzi Mwajuma Saidi Masaigana na kwamba alimtaka asikate tamaa katika kutekeleza majukumu yake.
  
Katika ziara yao wadau hao waliweza  kuona maonyesho mbalimbali kutoka kwa wanafunzi wa shule hiyo na kufurahishwa namna watoto hao walivyoweza  kuonyesha umahiri wao katika mambo mbalimbali.

Wadau wa elimu kutoka Ujerumani wakimsikilza mwenyeji wao, Mkurugenzi wa shule ya msingi  MWASAMA,  Mwajuma Saidi Masaiganah, hayupo pichani, kutoka kulia ni Bernd Sdiapers, wa pili kulia ni Agnes Weper na wa kwanza kushoto ni Sebasitian Schramm.

Walitembelea eneo lote lashule ili kujionea mambo mbalimbali katika shule hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa shule ya MWASAMA, Mwajuma Saidi Masaiganah, katikati ni Bernd Sdiapers, na wa kwanza kushoto ni Sebastian Schramm.

Wageni  hao walitembelea ujenzi wa bweni lawanafunzi, kushoto ni Makamo mwenyekiti wakamati ya shule hiyo, Hamza Mfaume anaefuata ni mwalimu mkuu wa shule hiyo Hamza Mapesa wakiwa na wageni wao.

Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Hamza Mapesa wa pili kushoto ni Makamo mwenyekiti wa kamati ya shule, Hamza Mfaume na mgeni wao Bernd Sdiapers



Kutoka kushoto ni Bernd Sdiapers, katika ni Sebastian Schramm na wa kwanza  kulia ni Agnes Weber wakiangalia michezo kutoka  wanafunzi wa shule hiyo.

Mkurugenzi wa shule ya msingi MWASAMA, akiwa na wageni wake wakiangalia wanafunzi wakinyesha michezo ya utamaduni.

Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) wakitoa burudani kwa wageni


Wanafunzi wa shule ya msingi MWASAMA wakitonyesha umahiri wao katika mambo utamaduni na sanaa mbele ya wageni


Wanafunzi wa KG nao wakifuatilia kinachoendelea.

Wanafunzi wa shule ya msingi MWASAMA  wakiimba  wimbo wa Tanzania Tanzania

Picha ya pamoja kabla ya kuondoka.


1 comment:

  1. Kutembelewa na maadili Hawa kumetupa faraja. Nd. Bernd Shoppers alikuwa Mwalimu wa sayansi kwenye iliyokuwa shule rafiki ya Real Schulle Shuleni ya Ujerumani. Aliwezesha wanafunzi wake kuchangisha fedha na kununua vifaa Vya sayansi Vya kufundishia wanafunzi wetu na kulea mtambo wa solar kwa gharama zao na mafundi wao.
    Shule ya Mwasamainavyo vifaa Vya kutosha na inakaribia Vyuo na vyuo vikuu Vya Bagamoyo vinavyotoa waalimu wa sayansi waje kufanyiwa mafundi kazini kwetu ili vifaa hivi viti Mike kwa taifa ya taifa hili. Mashirikiano katika sekta ya elimu ni muhimu katika kutoa elimu Bora na si Bora elimu. KARIBUNI sana tuijenge Tanzania yenye wanasayansi bora duniani.

    ReplyDelete