Saturday, October 8, 2016

UJENZI WA MSIKITI BOKO BEACH, MILIONI 3 ZAPATIKANA, INAHITAJIKA MILIONI 550.


 
Diwani wa kata ya Bunju, Kheri Nasoro alipokuwa katika harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiri.
....................................................

Harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiti katika mtaa wa Boko beach imefanikisha kukusanya milioni tatu na laki mbili, 3,200,000/= ikiwa ni pesa taslimu pamoja na ahadi huku Diwani wa kata ya Bunju Kheri Nasoro, akiwa amechangia kiasi cha shlilingi milioni moja katika ujenzi huo wa Msikiti.
Akizungumza katika Harambee hiyo iliyofanyika katika eneo linalotarajiwa kujengwa msikiti mtaa wa Boko beach Diwani wa kata Bunju Kheri Nasoro amesema atashirikiana na uongozi wa Swafatul mukarama ambao ndio wasimamizi wa ujenzi huo ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika.
Alisema wailsamu wanapaswa kutambua kuwa jambo hilo ni lao  na kwamba kila mmoja ajitolee kulingana na uwezo wake ili kufikia malengo.
Katika harambee hiyo mada za umuhimu wakutoa ziliwasilishwa ambapo Ustadhi, Hashim Rajabu kutoka Masjid Fatmat Zaharaa Boko, alisema waislamu wanapaswa kutambua kuwa kutoa katika njia ya kheri ni kujiwekea akiba ambayo itamsaidia mwenyewe siku ya malipo.
Akinukuu Hadithi ya  Mtume  Muhammad Swalallaahu Alayhi Wasallama, Ustadhi, Hasim alisema ''Mwenye kujnga msikiti, Mwenyezimungu atamjengea nyumba peponi'' hivyo aliwataka waislamu kukimbilia kheri hiyo kwaajili ya kutengeneza Akhera yao.
Nae Ustadhi Omari Jumakutoka masjid Rrahmani Tegeta, alisema swala la kutoa katika njia ya Mwenyezimungu linahita imani na wala si kipato kikubwa kama ambavyo wengi wanadhani.
Ustadhi Omari alitolea  mfano wa baadhi ya  matajiri wanaodhamini mashindano warembo na michezo ya mpira kwa gharama kubwa huku wakiwa hawana habari na  dini ya Allaah katika kuipigania.
Aliongeza kwa kusema kuwa swala la kutoa  katika njia ya mwenyezimungu ni  jihadi ndiyo mana katika  aya kadhaa  ndani ya Qurani Mwenyezimungu amesema kupigana jihadi kwa mali zenu na nafsi zenu, hii inonesha uzito wa  kutoa hali iliyopelekea  kuwekwa katika darja ya jihadi.
 Aliendelea kwa kusema kuwakila neema  itaulizwa, hivyo muislamu asidhani kwakumiliki kwake fedha anayo fursa ya kutumia anavyotaka, bali anapaswa  kutumia fedha kwa mujibu Allaah anavyotaka kwakuwa  kwake yeye zimepita kama  wakala hivyo ataulizwa namna alivyozitumia.
Akifunga  Harambee  hiyo, katibu wa Swafatul Mukarama Abduli Said Shomari alisema katika siku ya kwanza ya harambee hiyo wameweza kukusanya kiasicha shilingi mioni 3  na laki  mbili ikiwa fedha taslimu pamoja na ahadi.
Katibu huyo ametoa wito kwa waislamu kuendelea  kuchangia ujenzi huo wa  msikiti ambao utagharimu shilingi  milioni mia tano na arubaini na saba, laki moja themanini na nne mia sita na tano, hadi kukamilika kwake, 547,184,615/=
 Aidha, alitaja namba kwa watakaokuwa tayari kuchangia wanaweza kuchangia kupitia tigo pesa 0673 976336, Airtel money 0682982111, au akaunti benki, 003140405030001 Benki  ya Amana, akauti zote hizo zinajulikana kwa jina la Masjid Swafatul-Mukarama.

Kwa maelezo zaidi wasiliana kwa namba  0784070891 katibu wa Bodi amba 0713422774 Mwenyekiti namba 0713326287.

No comments:

Post a Comment