Saturday, October 22, 2016

DC BAGAMOYO, AINGIA GHAFLA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI KIWANGWA ABAINI SHIDA YA MAJI, UTORO WA WALIMU NA UVAMIZI WA MAENEO YA SHULE.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, kushoto Majidi Mwanga akikagua shule ya sekondari Kiwangwa, kulia ni makamo mkuu wa shule ya Sekondari Kiwangwa, Robadi Uzageni.
.............................


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majidi Mwanga atembela ghafla shule ya Sekondari Kiwangwa ili kuangalia utendaji kazi na changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo.

Katika ziara hiyo mkuu huyo wa wilaya aligundua mambo kadhaa, ikiwemo utoro wa walimu, upungufu wa matundu ya choo na tatizo la maji ambpo wanafunzi huchota maji umbali mrefu.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kitendo cha  kufuata maji umbali mrefu kwa wanafunzi  kuna matatizo kadhaa yanayowakuta ikiwa ni  pamoja na kuchelewa vipindi darasani, hatari ya kuviziwa na wavulana nje ya shule hali itakayopelekea wasichana kupata mimba na maumivu ya kubeba ndoo.

Wakizungumzia adha wanayoipata  katika kuchota maji wanafunzi hao wamesema kuwa wanatumia umbali mrefu kufuata maji na kwama wakifika kisimani kunakuwa na foleni kubwa kwakuwa kisima hicho hutumiana wananchi wengine hali inayopelekea kuchelewa masomo.

Wameongeza kuwa endepo mwanafunzi akifanya  kosa na akapewa adhabu ya kuchota maji atakaa siku nzima anachota maji kulingana umbali wa kufuata maji.

Aidha, wasichana katika shule hiyo pia wamekiri kuwepo kwa tabia za wanaume wa mitaani kutumia nafasi hiyo kuwasumbua njiani hali inayopelekea kuhofia usalama wao wa kiafya na kuharibikiwa kimasomo kwani wanaweza kuingia kwenye mapenzi bila ya kutarajia kutokana na mazingira.

Kwa upande wake makamo mkuu wa shule ya Sekondari Kiwangwa Robadi Uzageni, alikiri kuwepo kwa tatizola maji katika shule hiyo hali inayopelekea wakati mwingine kukatisha vipindi ili wanafunzi wakapate maji.

Alisema kutokana na halihiyo wakati wanafunzi hutolewa jioni kwnda kuchota maji na  huchukua muda mrefu kwenye foleni kutokana na umbali lakinipia visima hivyo hutumka pia na wananchi wa vijiji vya Bago na Kiwangwa hali inayopelekea wanafunzi  kukosa chakula kwakuwa hutumia muda mrefu kwenye maji  mpaka muda wakula unawapita wakiwa huko.

Mwalimu Uzageni alitumia nafasi hiyo kuwaomba wadau  mbalimbali wa maendeleo kuisadia shule sekondari kiwangwa ili ipate maji iweze kuondokana na adha ya kutafuta maji umbali mrefu jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa wanafunzi.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majidi Mwanga  amewaomba wadau mbalimbali kuchangia upatikanaji wa maji katika shule hiyo ili kuwaondolea adha  wanafunzi wanosoma katika shule hiyo.

Aidha, mkuu huyo wa wilaya ameishukuru Taasisi ya The Islamic  Foundation (TIF) yenye makao yake makuu mkoani Morogoro, kwa kusaidia visima katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Bagamoyo na kumuomba mwenyekiti wa The Islamic Foundation, Aref Nahdi kuangalia uwezekano wa kuwapatia maji shule ya sekondari Kiwangwa.

Taasisi ya The Islamic Foundation ya  mjini Morogoro ni miongoni mwa taasisi zilizochangia upatikanaji wamaji katika wilaya ya Bagamoyo ambapo kuanzia mwaka 2006 imeweza kuchimba visima 220 kati ya hivyo vipo virefu na vifupi ambavyo vimegharimu zaidi ya milioni 800. 

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga akisalimiana na wanafunzi wa shule ya Sekondari Kiwangwa huku  akiwasisitiza  kusoma kwa bidii.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akielekea katika kisima ambacho  wanafunzi wa shuleya sekondari wanapata maji, kushoto ni makamo mkuu  wa shule ya Sekondari  Kiwangwa, Robadi Uzageni.
 
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majidi Mwanga akiingia kwenye eneo la kisima ambacho wanafunzi wanachota maji.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, majidi mwanga akichota maji kwenye kisima kwa kutumia kata ya kuchotea.



Mkuu wa wilaya ya  Bagamoyo Majidi Mwanga akikokota Baiskeli kutoka kisimani hali ambayo wananchi wa  kijiji cha  Bago hutumia baiskeli kubebea maji.
 Wanafunzi wa shule ya Sekondari Kiwangwa wakitoka  kuchota  maji umbali mrefu kutokana na shule hiyo kukosa maji.





No comments:

Post a Comment