Friday, October 7, 2016

MAHAFALI YEMEN ENGLISH MEDIUM, WAZAZI WAONYWA MATUMIZIYA IPAD, SIMU KWA WATOTO



Wahitimu waelimu ya Msingi katikashule ya msngi ya  yemen iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Muasisi wa Shule za DYCCC Salim Baabae akizungumza  katika mahafali hayo

 ....................................................

Wazazi na walezi wametakiwa  kudumisha malezi bora  wanayopata watoto wao katika shule za kiislamu ili kuweza kupata Taifa lenye viongozi wenye  maadili katika jamii.

Wito huo ume umetolewa na muasisi wa shule za yemeni, Salim Baabae, alipokuwa akizungumza katika mahafali ya wahitimu  wa darasa la saba washule ya msingi Yemeni English Medium yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo iliyopo eneo la Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Salim  Baabae ambae ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika  mahafali hayo amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanadumisha malezi na tabia njema walizopata watoto wao walipokuwa shule ya msingi  ili malezi na tabia hizo ziendelee katika maisha yao yote.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kuwa makini na vitu vya kuwanunulia watoto wao ili kuepuka kuwanunulia vifaa vitakavyowatoa kwenye maadili na kupoteza malengo yao yabadae.

Alisema katika kipindi hikicha utandawazi, watoto wengiwamekuwa wanamiliki, simu, I pad, na mfano wa hivyo ambavyo kwa kiasi kikubwa vinachangia katika mmomonyoko wa maadili katika jamii huku vitu hivyo vikichangia katika kufeli kwa watoto kwakuwa muda  mwingi wanashughulishwa na matumizi ya simu na  I pad kuliko kufuatilia  masomo.

Aliongeza kwa kuwataka wazazi na walezi kuchagua shule zenye kutoa elimu bora kwaajili ya masom o ya sekondari ili wasipoteze taaluma waliyopata watoto wao ambapo aliwataka wazazi na walezi kuwaacha watoto katika shule ya sekondari ya Yemeni ili waendeleze taaluma namalezi bora waliyopata shuleni hapo. 
 
Nae mwenyekiti wa Bodi ya Shule, Hassan Akrabi, amesema mafanikio yaliyopatikana katika shule za  Yemeni ni kutokana  kuwa na  mahusiano  mazuri na jamii yote kwa  ujumla huku akitoa shukrani zake kwa vyombo vya Habari vya Imaan Media pamoja na uongozi wa The Islamic Foundation ukiongozwa na  Mwenyekiti  wake Aref Nahdi kwa kushirikiana katika fikra za  kupiga hatua  kimaendeleo.

Alisema Imaan Media pamoja  na TIF kwa ujumla imekuwa na mchango mkubwa hasa pale inapohitajika kutoa fikra za kimaendeleo ambapo mwenyekiti wake Arif Nahdi amekuwa mwepesi kuonesha ushirikiamno.
Mwenyekiti huyo wa Bodi ya shule aliwataka wazazi na walezi wa shule hiyo kuunga mkono juhudi zinazofanywa na uongozi wa shule ili kufikia malengo ya kuwalea watoto  kielimu na  kimaadili.

Alisema katika kuunga mkono juhudi ni pamoja na kulipa ada kwa wakati ili kuepuka watoto kurudishwa nyumbani kwaajili ya ada jambo ambalo linarudisha nyuma taaluma ya mtoto.

Awali akizungumza mbele ya mgeni rasmi mwalimu mkuu wa shule ya msingi Yemen English Medium, Rahimu Burhani, amesema shule hiyo imejipanga  kuboresha Taaluma ambapo mwalimu mmoja anafundisha watoto wasiozidi 30, ili kila  mtoto aweze  kuelewa vizuri anachofundishwa darasani.

Alisema shule  hiyo imejiandaa kuongeza wanafunzi zaidi kwakuwa tayari wanavyo vyumba vya  madarasa ambavyo havina wanafunzi na  kuwataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuwaunga  mkono kwa kupeleka watoto wao ili wapate elimu yenye manufaa.

Jumla ya wanafunzi 110 wamehitimu elimuya msingi katika  shule ya msingi ya Yemen ambao kati yao wavulana ni 48 na wasichana ni 62.
Jumuiya ya D.Y.C.C.C.  inamiliki shule shule yaawali, shule ya msingi, pamoja na shule ya  sekondari,



Baadhi ya wazazi wakiwa katikamahafalihayo
Mwen yekiti wa Bodi ya  shule za Yemen, Hassan  Akrabi  katikati, kushoto ni muasisi wa shule hizo Salim Baabae, na kulia ni mjumbe bodi Salmin  Aljabry.

Wanafunzi wa darasa   la  kwanza katika shule hiyo

Baadhi ya wazazi wakiwa katikamahafalihayo

Kulia ni mwenyekiti wa Bodi ya Shule za DYCCC Hassan Akrabi katikati ni muasisi washule za DYCCC Salim Baabae na kushoto ni mwalimu  mkuu wa shule ya Yemen English Medium, Rahimu Burhani.

Mgeni  rasmi, ambae ni muasisi wa shule za DYCCC Salim Baabae akimkabidhi zawadi mwanafunzi, kulia ni mwenyekiti wa bodi ya shule Hasan Akrabi, na wa kwanza kushoto ni mkuu wa shule hiyo Rahimu Burhani
Sehemu ya majengo ya shule za DYCCC eneo la Chang'ombe jijini Dar es Salaam.






No comments:

Post a Comment