Saturday, July 30, 2016

KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA ZA WILAYA NNE ZATOKA NA MAAZIMO 10 BAGAMOYO, KUHUSU MSITU WA ZIGUA.

Mwenyekiti  wa Mkutano huo, ambae  ni Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga.


Mkutano wa kamati za ulinzi na usalama za wilaya nne uliofanyika mjini Bagamoyo kuhusu wavamizi wa msitu wa Zigua, umetoka na maazimio 10, ambayo yanatakiwa kutekelezwa.

Mkutano huo uliozijumuisha kamati za ulinzi na usalama za wilaya nne ambazo ni Bagamoyo, Mvomero, Kilindi na Handeni, umefanyika mjini Bagamoyo ili kujadili namna ya kuwaondoa wavamizi waliovamia msitu wa Zigua.

Awali akiwasilisha mada mbele ya mkutano huo meneja wa Wakala  wa Misitu Tanzania TFS wilaya ya Bagamoyo, Charles Mwafute, alisema wameamua kushirikisha kamati za ulinzinausalama za wilaya hizo zinazopakana na hifadhi ya msitu wa Zigua ili kupata ushirikiano wakutosha katika kukabiliana na wavamizi.

Nae Mwenyekiti wa Mkutano huo Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed Mwanga aliwataka viongozi wote katika wilaya hizo kuelimisha jamii juu ya utunzaji wa misitu ikiwa ni pamoja na kupanda miti mipya ili jamii iendelee kuwa na misitu.

Baada ya majadiliano mkutano huo umetoka na maazimio 10 ambayo yanatakiwa kutekelezwa kwa manufaa ya Taifa ili kuunusuru msitu wa Zigua nayo ni:

1.   Kuwaondoa wavamizi wote ndani ya  hifadhi  ya  msitu ifikapo Tarehe 30 Septemba 2016.

2.   Kila wilaya  itambue maeneo yaliyovamiwa.
3.   Mtu yeyote aliyeshiriki, au atakaeshiriki kugawa maeneo ndani ya Hifadhik achukuliwe hatua za  kisheria.

4.   Kuunda kikosi kazicha kufuatilia maeneo yaliyovamiwa na kutoa taarifa kamati.

5.   Kuanzisha Doria  za mara kwa mara  ndani ya hifadhi kwa wilaya zote nne  mara baada ya kuwatoa wavamizi.

6.   TFS, izingatie utoaji wa motisha kwa watakaoshiriki katika doria na watakaotoa taarifa  za wavamizi.

7.   Mipaka iendelee kuimarishwa kwa kushirikisha jamii inayozunguuka hifadhi.

8.   Kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa hifadhi ya msitu kabla na baada ya kuwaondoa wavamizi.

9.   Katika  kuwaondoa  wavamizi sheria izingatiwe.
10.                Kuweka walinzi wa misitu baada  ya kuwaondoa wavamizi.
Mkuu wa wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe.
Mkuu wa wilaya  ya Mvomero, Mohamed  Utaly.
 
Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mwl. Sauda Mtondoo.


No comments:

Post a Comment