Thursday, July 21, 2016

BENKI YA AMANA YAZINDUA HUDUMA MPYA KWA WATEJA, KWA NJIA YA SIMU (CALL CENTER).

Meneja mfawidhi huduma kwa wateja, Juma  Msabaha, akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu huduma ya Call Center.


Benki ya Amana imezindua huduma mpya kwa wateja wake, kwa njia ya simu (Call Center) iliyopewa jina AMANA  BANK MTAANI, lengo likiwa ni kuboresha huduma kwa wateja wa Benki hiyo inayofuata sheria ya kiislamu hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika uzinduzi wa huduma hiyo, uliofanyika makao makuu ya benki ya Amana jijini Dar esSalaam, Meneja Mfawidhi, huduma kwa wateja, Juma Msabaha, alisema lengo la huduma hiyo mpya iliyopewa ni kuwasogelea wateja ili  kuboresha huduma.

Alisema huduma itapatikana kwa muda wa masaa 15 kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 4 usiku ambapo katika muda huo wateja wataweza kupiga simu na kuongea na muhudumu, anaetoa huduma kwa wateja moja kwa moja.

Aliongeza kuwa kupitia huduma hiyo mteja anaweza kuuliza swali lolote linalohusu huduma za Benki ya Amana na kupata ufafanuzi bila ya  kulazimika kufika kwenye tawi Benki ya Amana.

Aidha, Msabaha, alizitaja namba za kupiga ilikupata huduma hiyo ni 0657980000 ambapo mawakala wa Call Center watajibu  maswali  mbalimbali yanayohusu huduma za Benki ya Amana ikiwemo aina za Akaunti za Benki ya Amana, kuhusu huduma za kibenki kwa njia ya simu, mikopo na huduma mbalimbali.

Nae mkuu wa Kitengo  cha Biashara   Munir Rajabu, alisema  Benki ya Amana imejipanga  kuboresha  hudama zake ambapo kwa mwaka  huu wameongeza kasi ya kuwafikia  wateja  kwa  kuweka  mawakala katika  maeneo mbalimbali ya nchi.

Alisema kitengo hicho cha Call Center kitarahisisha huduma kwa wateja hasa katika maeneo ambayo Benki ya Amana  haina matawi ambapo ni vigumu mteja kufika kwenye matawi na kwa sasa mteja atapata huduma  kupitia mawakala watakaowekwa nchini kote.

Katika kipindi cha miaka mitano, Benki ya Amana imeweza kuwa   na matawi saba, ambapo matawi  matano yakiwa  katika jiji laDar esSalaam, moja likiwa Arusha na moja Mwanza, huku kauli mbiu yao ikiwa ni wateja kwanza.     

Mkuu wa kitengo cha biashara Benki ya Amana, Munir  Rajab akizungumzana waandishi waHabari.
 
Kutoka kushoto ni meneja wa Tawi la makao makuu, Aisha Awadhi, katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara, Munir Rajabu, na kulia ni Meneja  Mfawidhi Huduma kwa wateja, Juma Msabaha.

Kutoka kushoto waliosimama, Mkuu wa Kitengo cha mikopo, Mzee Muhsin, wa pili ni Mkuu wa kitengo cha Bidhaa na sharia, Muhsin Mohamed na watatu ni Mkuu w kitengo  cha uajiri Shabani Diwani,  waliokaa, kutoka kushoto  ni Meneja  wa Tawi la Makao makuu, Aisha Awadhi, anaefuata ni Mkuu wakitengo cha Biashara, Munir Rajabu, na wa mwisho kulia ni Meneja Mfawidhi huduma kwawateja, Juma Msabaha.

No comments:

Post a Comment