Thursday, July 14, 2016

JK. AFUNGUA MKUTANO WA TATU WA MABADILIKO YA TABIA NCHI JIJINI DAR ES SALAAM.



Rais mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa tatu wa Sera za Mabadiliko ya Tabia Nchi jijini Dar es Salaam iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Climate Strategies. Mkutano huo ilijumuisha watafiti na watunga sera 80 kutoka nchi zaidi ya 10 nje na ndani ya Afrika chini ya kauli mbiu "Kutekeleza Makubaliano ya Paris - Suluhu Mpya za Utafiti kwa ajili ya Nchi zinazoendelea." Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa mkutano huo Bw. Chuks Okereke, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mhe. January Makamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja. 

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mhe. January Makamba akizungumza katika mkutano wa tatu wa Sera za Mabadiliko ya Tabia nchi unaoendelea jijini Dar es Salaam. Waziri Makamba amesema kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi 175 zilikubali na kutia saini Makubaliano ya Paris Aprili 22 mwaka katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York ili kuweza kupunguza na kudhibiti utoaji wa gesi ya kaboni duniani. 
 

Mwenyekiti wa Mkutano wa Sera za Mabadiliko ya Tabia Nchi Bw. Chuks Okereke kutoka Chuo Kikuu cha Reading, Uingereza akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Mkutano huu ni wa tatu kufanyika duniani na wa kwanza kufanyika barani Afrika baada ya London, Uingereza 2014 na New Delhi, India 2015.

No comments:

Post a Comment