Saturday, July 23, 2016

HOSPITALI YA KIMATAIFA YA MACHO YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.

Mjumbe wa Hospiatali ya Kimataifa ya Macho, Aliy Daric akisoma risala mbele ya wageni waalikwa, katika hiyo ya The  International Eye Hospital iliyopo  maeneo Victoria jijini Dar es Salaam.


Waislamu na watanzania kwa ujumla wametakiwa kujenga tabia ya kupima  macho mara kwa mara ili kuyapatia matibabu ikiwa yatagundulika  kuwa na matatizo.

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam, na Amiri wa shura ya maimamu nchini, Sheikh Musa Kundecha alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa Hospitali ya kimataifa ya Macho iliyopo jijini  Dar es Salaam.

Sheikh Kundecha ambae  alikuwa mgeni rasmi, alisema Macho ni kiungo muhimu kwa binadamu katika kuendesha shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na ibada ikiwemo usomaji wa Qur ani.

Alisema, waislamu wanapaswa kuwa na tabia ya kupima magonjwa mbalimbali huku akisisitiza swala la upimaji wa macho kwakuwa  umuhimu wa macho ni mkubwa katika kufanikisha mambo mbalimbali.

Aliongeza kuwa watu wengi  wanavaa miwani bila ya kupima jambo ambalo ni hatari kwakuwa miwani hutengenezwa kwa vipimo kulingana na nguvu ya  macho ya muhusika hivyo kitendo cha kuvaa miwani bila ya kupima ni kujiongezea matatizo.

Awali akisoma risala mbele mgeni rasmi mjumbe wa Hospitali hiyo ya kimataifa ya  Macho, aliy Daric, alisema ujenzi wa Hospitali hiyo hapa nchini umetokana na  mahitaji ya jamii, ambapo imebainika katika nchi za  Afrika kuna uhaba wa Hospitali zinazotoa matibabu ya macho hasa ukilinganisha na ukubwa wa tatizo la Macho.

Alisema Hospitali hiyo ilianzishwa mwaka 2013 na kuanza shughuli zake za tiba mwaka 2014 ambapo imeweza  kuwatibu viongozi mbalimbali wa serikali, masheikh na wa Taasisi mbalimbali lengo likiwa ni kutoa huduma sahihi na yenye ubora.

Nae Mkurugenzi wa masoko katika Hospitali hiyo, Adama Mwatima, ametoa wito kwa jamii kuitumia Hospitali hiyo ili kupata matibabu ya Macho  hasa ikizingatiwa kuwa Hospitali hiyo ina wataalamu na vifaa vya  kisasa  katika kutibu macho.
Mmoja wa watendaji wa Hospitali hiyo akiwaonesha Masheikh baadhi ya vyumba vya Hospitalihiyo.
Baadhi ya watendaji katika Hospitali hiyo
Rais waHospitali hiyo, Fatih Gunan akiwaeleza wageni waalikwa namna wanvyofanya kazi katika Hospitali hiyo
Baadhi ya Madaktari katika Hospitali  hiyo The International Eye Hospital iliyopo jijini  Dar es Salaam nchini  Tanzania
Sheikh Musa Kundecha, katikati akielezea jambo wakati wa kupata chakula katika hafla ya uzinduzi wa Hospitali ya Kimataifa ya Macho iliyopo Victoria jijini Dar es Salaam.


            





   

No comments:

Post a Comment