Sunday, July 31, 2016

MOTO WATEKETEZA GODAONI LA KUHIFADHIA MATAIRI DAR.

 
Godaoni la kuhifadhia mataili pamoja na vifaa vinginevyo vya magari lililopo Sinza Lego ambalo mmiliki wake hakufahamika mara moja, limeteketea kwa moto ambapo kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa chanzo cha moto huo ni mataili, mpaka jioni hii kikosi cha kuzima moto kilikuwa eneo la tukio kuendelea kusaidiana na wananchi katika  kuzima  moto huo, Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi.
 
Godaoni linalosadikiwa kuhifadhi vipuri vya magari likiwa linateketea kwa moto jioni hii Sinza Lego jijini Dar es salaam ambapo juhudi za kuzima moto zinaendelea japokuwa kazi ya kuzima imekuwa ngumu kutokana na aina ya vipuri vinavyohifadhiwa katika ghala hilo kuwa aina ya mipira na mafuta ya vilainishi vya vipuri.
 

Moto ukiwa umeshika kasihuku juhudi za kuuzima zikiendelea

No comments:

Post a Comment