Sunday, July 31, 2016

DAR ES SALAAM NATURE STUDY, KITUO CHA MAARIFA.

Suleiman kuliwa, akitoa somo kwa wanafunzi wa shule ya wasichana ya Lukman ya jijini Dar es Salaam, mara walipotembelea kituoni hapo kujifunza ma mbo  mbalimbali.
Mwalimu Yasini Mkwizu akitoa ufafanuzi kuhusu aina mbalimbali za miti na faida zake mbele ya wanafunzi wa shule ya Lukmani walipotembelea eneo hilo ambapo waliweza  kujifunza  mambo mbalimbli ikiwemo umuhimu wa kuhifadhi misitu.
Ukiwa Dar es Salaam Nature  study  unaweza  kufahamu majina ya miti mbalimbali na faida  zake.
Wanafunzi wa shule ya Lukmani ya Sinza jijini Dar es Salaam wakionekana  kwa mbali katikati ya msitu  wakijifunza mambo mbalimbali  walipokuwa katika  ziara ya kimasomo katika msitu huo unaohifadhiwa na kituo cha Dar es Salaam Nature Study.

Mwalimu, Sadiki Kizuki, ambae ni mwalimu wa Jografia  na Historia akiwapa somo wanafunzi wa shule ya sekondari Chamanzi mife walipotembelea katika hifadhi ya msitu wa Dar Nature Study ili kujifunza  mambo mbalimbali.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Chamanzi mife wakimfuatilia mwalimu Sadiki Kizuki hayupo pichani, walipokuwa katika kituo cha Mpopoma, baadae  walielekea mto Nyebulu kisha kupanda Mlima wa Togwa lengo likiwa kujifunza  mambo mbalimbali.
Mwalimu Sadiki, mwenye  miwani akiwapa  somo  wanafunzi wa Chamanzi Mife.
Ukifika  Dar es Salaam Nature Study,  utakutana  na  mwalimu  huyu, mwalimuSadiki Kizuki mtaalam wa Jografia, Historia na elimu ya viumbe.

No comments:

Post a Comment