Thursday, August 3, 2023

WAZAMIAJI HARAMU 4, WALAZIMIKA KUNYWA MAJI YA BAHARI ILI WAENDELEE KUISHI.

Wazamiaji haramu 4 wa Nigeria walazimika kunywa maji bahari kwa siku nne ili waendelee kuishi baada ya kudhani wanaenda bara la Ulaya na bila kutarajia wakajikuta wapo bara la America nchini Brazil


Wakihojiwa na shirika la Reuters, mmoja amesema siku ya kuzamia alisaidiwa na rafiki yake mvuvi kumpeleka kwenye meli husika ya mizigo, ila alipoingia kinyemela chini katika rudder ya meli akakutana na Wanigeria wenzie wengine watatu ambao hakuwa akiwafahamu hivyo akaanza kuingiwa na hofu kuwa watamuua kwa kumtosa baharini


Lakini, meli ilipoanza kuondoka wote wakakubaliana watulie kimya ili wafanyakazi wa meli wasije wakawagundua na kuwaua kwa kuwatosa baharini wote


Mmoja wa wazamiaji hao kwa jina la Friday amesema ilikuwa ni safari ya hatari sana kwao hasa eneo la rudder ya meli walipokaa maana hata mtu kulala na kujisahau ilikuwa ngumu unaweza ghafla kujikuta tayari umeangukia baharini bila kutarajia hivyo walifunga neti katika eneo husika na wao wote kujifunga kamba ili yeyote kati yao asije kutumbukia baharini kimakosa maana kuna muda wakiwa kwenye hiyo neti chini yao walikuwa wanaona viumbe hatari vya baharini wakiwemo papa na nyangumi 


Alianza safari tarehe 27 June mwaka huu na amesema siku ya kumi wakiwa ndani ya meli  vyakula na vinywaji walivyokuwa wamebeba viliwaishia hivyo ilibidi kwa siku nne wanywe tu maji ya bahari maana meli ilichukua wiki mbili kufika Brazil huku wakiwa hoi kwa njaa na kutopata usingizi


Amesema walipokuja kuokolewa alijisikia furaha badala ya hofu maana safari yao yenyewe ikiwemo eneo walilokaa kwa siku zote ilikuwa hofu tu muda wowote mtu anaweza poteza maisha


Hata hivyo, walikamatwa nchini Brazil ambapo wawili kati yao kwa hiari yao wameomba kurudishwa nchini mwao Nigeria na tayari wamesharudishwa, ila wawili waliobaki akiwemo Friday na mwenzie wao wamejaribu kuomba hifadhi maalum ya kikimbizi(asylum) ili wabaki nchini Brazil ingawa bado maombi yao hayajibiwa 


Amesema wana matumaini serikali ya Brazil itawaonea huruma na kuwajibu wakae nchini humo akisema kwamba yeye ana familia na amekimbia nchi yake Nigeria kwasababu ya hali ngumu ya kiuchumi, migogoro ya kisiana na uhalifu kuzidi akisema ana familia ambayo inamtegemea na hali yake ya kiuchumi ni ngumu na alikuwa analima shamba lakini mafuriko yaliharibu kila kitu.


Miongoni mwa wazamiaji hao wana miaka zaidi ya 35


Kiongozi mmoja wa kidini nchini Brazil amewatembelea wazamiaji wa nchi mbalimbali wanaoingia kinyemela Brazil ila wazamiaji wa Nigeria huwa na safari hatarishi zaidi






 

No comments:

Post a Comment