Thursday, August 3, 2023

DC OKASH ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA BAGAMOYO NANENANE MOROGORO, AHIMIZA WAJASILIAMALI KUTAFUTIWA MASOKO YA UHAKIKA.

 


Na Nurdin Ndimbe, Morogoro.



Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash ametemblea banda la 

Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo katika maadhimisho ya maonesho ya wakulima 

Nanenane 2023 yaliyofunguliwa leo tarehe 1 Agosti, 20223 katika viwanja vya 

kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Manispaa ya Morogoro.


Akizungumza na wajasiliamali katika banda hilo, aliwaomba wajasiliamali kutengeneza bidhaa zenye ubora ili kupata soko la uhakika na kujiongezea mapato ya mtu mmoja mmoja na Halmshauri kwa ujumla wake. 


Aileleza kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Daktari. Samia Suluhu Hassan ipo pamoja katika kuwatafutia mitaji ya biashara na kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara zao.


“Napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwenu kwa kujituma na kuja kwenye maonesho haya, hatua hii ni muhimu kwenu kwa ajili ya kujitangaza na  kupata masoko ya uhakika masoko lazima yatafutwe kwa njia zote. Alisema Mhe, Okash.



Aidha Mhe.Okash aliuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Bagamoyo 

kuwatafutia masoko ya uhakika wajasiliamali hao, ili kukuza kipato chao na 

kuendeleza miradi yao. 


Alihaidi kuwa, baada ya maonesho ya Nanenane atapanga kikao maalumu cha kukutana nao ili kujadili kwa kina fursa zilizopo kwa wajisiliamali wadogo Bagamoyo na changamoto zinazowakabili ili kupata ufumbuzi wake.” Nihahidi 

tuu baada ya Nanenane tupange tuonane, kuona uwezekano wa nyinyi kupata 

maeneo ya kuzalishia na kuuza bidhaa zenu”. Alisisitiza.


Kwa upande wao wajasiliamali hao walisema kuwa changamoto kubwa ni 

ukosefu wa masokao ya uhakika hata hivyo, walimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa 

kuwatembelea na kujionea bidhaa zao katika maonesho haya ya Nanenane.



Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Nane nane 2023 “ Vijana na Wanawake ni msingi 

imara wa mifumo endelevu ya chakula.





 




No comments:

Post a Comment