Thursday, August 3, 2023

KIPANGA AONGOZA KONGAMANO LA TIMU YA WATALAAMU WANAOTAKA KUJA KUWEKEZA NCHINI WANAOKUTANA RWANDA

KIGALI-RWANDA*


Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknologia Mhe Qs Omar Kipanga ameongoza timu ya wataalamu wanaotaka kuja kuwekeza Tanzania katika sekta mbalimbali nchini walipokua Kigali Rwanda,


Akiziungumza wakati wa kongamano Hilo Mhe Qs Omar Kipanga amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na vyanzo mbalimbali ambavyo vinahitaji kuendelezwa ili jamii ipate faida navyo Hivyo kupitia hapo wawekezaji wanapata kufahamu Maeneo gani Wao wanahijaji Hivyo ni muhimu kuelekezwa alifafanua Mhe Qs Kipanga


*"Hapa Kigali Rwanda tunakutana Wajumbe kutoka Tanzania na nchi mbalimbali zikiwemo hizi za afrika Mashariki na Ulaya Hivyo basi ni muhimu kuelekezwa kwao waweze kuja kwetu kuwekeza maana Serikali ya RAIS Dkt Samia Imeweka Mazingira Mazuri ya Uwekezaji na uendelezaji wenye tija kwa Taifa alimalizia Mhe Qs Kipanga*"


Washiriki wa Tanzania katika kongamano la Afrika la Usalama Mitandaoni linalofanyika Kigali, Rwanda wakiwemo kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), kampuni ya masuala ya usalama mitandaoni ya CHIKITO na Umoja wa WanaTEHAMA Afrika (AfiCTA) wakiongozwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omari Kipanga, wameshiriki vikao na wawekezaji kutoka nchi za Romania na Israel, kwa lengo la kushirikiana katika masuala ya TEHAMA na Usalama mitandaoni.


Baada ya vikao hivyo, hatua itakayofuata ni kurasimisha mazungumzo hayo ya ushirikiano baina ya Tanzania na wawekezaji hao, na kisha kuweka bayana makubaliano yaliyofikiwa. 




Washiriki wa Tanzania katika kongamano la Afrika la Usalama Mitandaoni linalofanyika Kigali, Rwanda wakiwemo kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), kampuni ya masuala ya usalama mitandaoni ya CHIKITO na Umoja wa WanaTEHAMA Afrika (AfiCTA) wakiongozwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omari Kipanga, wakiwa katika vikao na wawekezaji kutoka nchi za Romania na Israel, kwa lengo la kushirikiana katika masuala ya TEHAMA na Usalama mitandaoni.







 

No comments:

Post a Comment