Thursday, August 3, 2023

WATU WANNE WAFARIKI AJALINI WILAYANI BAGAMOYO.


Na Athumani Shomari- Pwani
 

Watu wanne wamefariki dunia baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso usiku wa kuamkia leo Agosti 03, 2023 wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani.



Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Mapatano, Kata ya Mbwewe, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoani Pwani, imepoteza maisha ya Mkurugenzi wa Benki ya ABSA na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Tawi la Dar es Salaam.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Pilisi, ACP.  Pius Lutumo amethibitisha tukio hilo katika Taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari.


Taarifa hiyo ya jeshi la polisi imesema kuwa ajali hiyo ilitokea jana Agosti 2, saa 2:30 usiku, ikihusisha gari aina ya Toyota Prado yenye namba ya usajili T.104 CBU, likitokea Dar es salaam kuelekea wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro, lililokuwa likiendeshwa na Nechi Msuya, na Scania yenye namba za usajiki T. 881 DWU / T.888 DWU lililokuwa likitokea Arusha kuelekea Dar es salaam, likiendeshwa na Philipo Mtisi mkazi wa Mafinga.



Waliofariki kwenye jali hiyo  wametajwa kuwa ni Nechi Msuya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 45 hadi 50, Dayana Mageta, mfanyabishara na makazi wa Dar es Slaam anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40 hadi 45, Nora Msuya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40 hadi 45 ambaye ni mwalimu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Tawi la Dar es Salaam, na abiria wa kike ambaye jina lake halikufahamika na anakadiriwa kuwa na miaka 30 hadi 35.


Jeshi la polisi limesema  chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Toyota Prado kuhama kutoka upande wa kushoto wa barabara kwenda upande wa kulia kisha kogongana uso kwa uso na lori hilo.



Jeshi la Polisi mkoani Pwani limetoa wito kwa madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kusababishwa na uzembe.




 









No comments:

Post a Comment