Thursday, June 13, 2019

BODI YA KOROSHO YATOA MAFUNZO YA VIUATILIFU LINDI.

NA HADIJA HASSAN- LINDI

KUTOKANA na matumizi madogo ya viuwatilifu vya zao la korosho uliojitokeza katika Msimu wa mwaka 2018/2019 Bodi ya korosho Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Kilimo Naliendele pamoja na TPRI imeanda mafunzo ya matumizi sahii ya viuwatilifu hivyo katika Mikoa yote inayolima zao hilo Hapa Nchini

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Francis Alfred alipokuwa akitoa salamu za bodi hiyo katika uzinduzi wa mafunzo ya Matumizi ya Viuwatilifu yaliyofanyika katika kata ya Maumbika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani Humo

Alisema matumizi hayo madogo ya viuwatilifu yamechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa uzalishaji wa zao hilo kutoka tani laki 313,000 za mwaka 2017/2018 hadi tani laki 214000 kwa mwaka 2018/2019.

Alisema mafunzo hayo hasa yanalenga makundi matatu ambayo ni wakulima wa zao la korosho, wapuliziaji wa viuwatilifu pamoja na maafisa ugani ambao baada ya mafunzo hayo watatakiwa kuwafundisha watu wengine katika makundi yao ambao hawakupata fursa ya kushiriki katika mafunzo hayo.

Alfred aliongeza kuwa Bodi ya korosho kwa kutambua uhaba wa maafisa ugani iliona njia sahihi ya kuwafikia wakulima hao kwa wingi na haraka zaidi ni kuyakutanisha makundi hayo na kuyapa mafuzo kwani wamekuwa wakipokea malalamiko mengi kutoka kwa wakulima kutokujua kiwatilifu sahihi kwa ugonjwa sahihi

Nae kaimu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya utafiti wa Kilimo Naliendele DKT, Fortunus Kapinga alisema katika mafunzo hayo washiriki watapata fulsa ya kujifunza njia na namna bora ya kutumia viuwatilifu, namna ya utunzaji bora wa viuwatilifu pamoja na jinsi ya kujilinda na viwatilifu hivyo ili usipatwe na madhara wakati wa kuvitumia

Hata hivyo DKT Kapinga alitumia fulsa hiyo pia kuishauri Bodi ya korosho kuendelea na utaratibu wa kuwa na mafunzo maalumu kwa maafisa ugani kila mwaka ili kukabiliana na magonjwa mbali mbali yanayoweza kuibuka katika misimu ya zao hilo

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Godfrey Zambi alisema pamoja na mafunzo wanayotakiwa kupatiwa washiriki hao pia wawafundishe jinsi ya kutunza Mazingira ikiwa pamoja na Namna ya kuteketeza vifungashio ambavyo vilitumika kuwekea viuwatilifu huku akiwataka watumiaji wa viwatilifu hiyo kutotumia vifungashio hivyo kwa matumizi ya nyumbani

“viuwatilifu vingi vinavifungashio, kunamifuko ya viuwatilifu vya unga, kunachupa kubwa na ndago, tunajiuliza baada ya kupuliza tunatupa wapi? Yapo mashamba ukizunguka unakutata na chupa zimetupwa hovyo, unakutana na mifuko tena mbaya zaidi hii mifuko tukimaliza kupulizia tunaiyosha alafu tunatiliamaindi tunaenda kusaga wengine wakimaliza kupuliza chupa anaosha anaweka chuvi au sukari.

Naomba tusaidiane baada ya kuwa tumetumia viuwatilifu vifungashio hivi tunavitupa wapi?” alieleza Ndemanga

Hata hivyo Ndemanga alitumia fulsa hiyo kuzitaka mamlaka zinazohusika na usambazaji wa viuwatilifu kufanya udhibiti wa uuzwaji holela wa viuwatilifu pamoja na maeneo yanayotumika kuuzia viuwatilifu ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza

Nae ibrahimu Ngalondola akizungumza kwa niaba ya wakulima wengine alisema kuwa miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo katika zao hilo ni bei kubwa ya viuwatilifu jambo ambalo huchangia kwa kiasi kikubwa kwa wakilima hao kushindwa kuandaa mashamba yao kwa wakati

No comments:

Post a Comment