Sunday, June 30, 2019

TRUMP AKUTANA NA KIM NA KUFANYA MAZUNGUMZO.

Rais Donald Trump wa Marekani amekutana na kiongozi wa Korea Kaskazini katika eneo lisilo la kijeshi la mpaka wa Korea mbili ambapo viongozi hao wawili walipeana mikono kuonesha ishara ya matumaini ya amani.


Rais wa Marekani Donald Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, wamekubaliana kuanzisha tena mazungumzo ya nyuklia yaliyokwama hapo awali.


Katika wiki zijazo, vikosi kazi vitaanzishwa kutoka pande zote mbili ili kuanza ukurasa mpya wa kuendeleza amani.


Upande wa Marekani utaongozwa na Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo.


Trump hakutoa maelezo zaidi kuhusu yale yatakayojadiliwa lakini ameeleza wazi kwamba vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini vitaendelea kubaki kwa muda mpaka hapo itakapofikiri vinginevyo.


Marekani imeitaka Korea Kaskazini isimamishe kabisa mpango wake wa nyuklia.


Korea Kusini na Marekani pia wanahimiza upatikane mkataba rasmi wa amani kati ya Korea Kusini na Kaskazini.

No comments:

Post a Comment