Sunday, June 2, 2019

WAKAZI PWANI WATAKIWA KUONGEZA UPENDO

Na Omary Mngindo, Kibaha.


WAKAZI Mkoa wa Pwani wametakiwa kuendeleza umoja, upendo na mshikamano, ambao hauna ubaguzi wa dini ya aina yeyote.


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo, katika futari iliyoandaliwa na mmiliki wa shule ya KIPS iliyoko Kibaha Mailimoja mkoani hapa Alhaj Yusufu Mginanga ambae pia ni mmiliki wa hoteli Njuweni.


Alisema kwamba dini imeendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya haraka nchini, kutolana na viongozi wake kuwahimiza waumini wake katika kuzingatia upendo, umoja na mshikamano na kuondoa utofauti ambao zinaambatana na udini.


"Nawapongeza viongozi wa dini mkoani Pwani, baadhi yenu hivi karibuni tumesafiri kwenda kujionea mradi mkubwa wa umeme wa maji Mto Rufiji, unaotekelezwa na serikali chini ya Rais Dkt. John Magufuli, nawapongeza kwa kazi zenu za kuhimiza amani, umoja, upendo na mshikamano," alisema Mhandisi Ndikilo.


Aliongeza kwamba mradi huo unaotaraji kuinufaisha nchi yetu katika kuhakikisha kunakuwepo na umeme wa uhakika, amewaomba viongozi wa dini wamuombee Rais aendelee kuwa na afya njema, pia kwa kazi kubwa ya kuuanzisha mradi huo ulioasisiwa na watangulizi wake.


"Wakoloni hawakuupenda mradi huu, sababu kubwa ni kwamba wamejua ungeleta maendeleo makubwa katika nchi yetu ya Tanzania, hivyo hatua ya Rais Magufuli kuuendeleza ni kitendo cha ujasili wa hali ya juu, tuanapaswa kuunga mkono kwa kazi hiyo," alisema Mhandisi huyo.


Kwa upande wake mkurugenzi wa Kampuni hiyo Alhaj Mfinanga amewataka wakazi mkoani hapa, pasipo kujali itikadi zao za dini, rangi wala siasa katika kuhakikisha kila mmoja anamsaidia Rais Magufuli katika utekelezaji wa ujenzi wa nchi, huku akisisitiza elimu.


Akizungumzia shule ya KIPS, Mfinaga alisema kwamba ilianzishwa mwaka 2002 ikiwa ni shule ya awali na msingi, ambapo tangu kipindi hicho inaendelea na utoaji wa elimu na kwamba wanafunzi wanafanya vizuri katika mithihani yao ya kuingia kidato cha kwanza.


Baadhi ya waumini wa dini waliohudhulia futari wamemshukuru mmiliki wa shule hiyo, huku wakimhaidi Mkuu wa Mkoa kwamba wataendelea na utoaji wa elimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo kudumisha amani, umoja, upendo na mshikamano.

No comments:

Post a Comment