Sunday, June 2, 2019

JUMAA ASAIDIA PWANI POLISI VIFAA VYA UJENZI

MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani Humoud Jumaa, akimkabidhi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP. Wankyo Nyigesa, risiti iliyonunuliwa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni 2.8.
.................................................... 

Na Omary Mmgindo, Kibaha.

MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani Humoud Jumaa, amekabidhi Jipsam 100 na ndoo tano za rangi vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 2.8.


Katika hafla fupi iliyofanyika eneo linalojengwa nyumba 20 za jeshi hilo mkoani Kibaha mjini hapa, Jumaa amemkabidhi Kamanda wa jeshi hilo Wankyo Nyigesa Jipsam hizo, kwa ajili ya ujenzi huo unaolenga kuwaweka pamoja askari hao.


"Nilikuja nikakutana na Kamanda Nyigesa kanielezea mikakati ya ujenzi wa nyumba 20 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali chini ya Dkt. John Magufuli inayotazama sekta zote, ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani, leo nimekabidhi jipsam na ndoo za rangi za sh. Mil. 2.8,


"alisema Jumaa. Alisema kuwa anapongeza jeshi hilo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wilayani hapa na Mkoa kwa ujumla wanaishi kwa amani, upendo na mshikamano mkubwa ambao unachangiwa na uwepo wa askari Polisi.


"Nimpongeze Rais Dkt. John Magufuli kwa uongozi wake unaojali maendeleo ya watu wake, tunashuhudia inavyoboresha sekta zote zikiwemo elimu, afya, miundombinu, umeme na ulinzi na usalama tunatakiwa kumuunga mkono kwa vitendo," alisema Mbunge huyo.


Kwa upande wake Kamanda Nyigesa alisema kwamba kwa sasa ili kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwezi wa sita, wanahitaji kiasi cha zaidi ya sh. Mil. 20 ili kukamilisha zoezi hilo, huku akiwaomba wadau zaidi wajitokeze katika kukamilisha mchakato huo.


"Niwaombe wabunge wengine na wadau mbalimbali wajitokeze katika kuunga mkono serikali yetu katika kuboresha masuala ya kimaendeleo kwenye nyanja zote," alisema Nyigesa. "


Tunapokea misaada kutoka kwa watu mbalimbali paaipokujali itikadi za kisiasa, polisi wananchi wote weti pasipokujali itikadi zao za kisiasa," alimalizia Kamanda Nyigesa.

No comments:

Post a Comment