Tuesday, June 18, 2019

WANANCHI LINDI WAHAMASISHWA KUCHANGIA DAMU.

Mkazi wa anispaa ya Lindi Juma Bakari akichangia damu katika moja ya vituo vya kutolea damu mjini humo.

NA HADIJA HASSAN, LINDI

Kundi la akinamama wajawazito na watoto wachanga limetajwa kuwa ndio kundi kubwa lenye mahitaji ya Damu salama katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Lindi sokoine.

Hayo yamebainishwa na mtaalamu wa Maabara wa Hospitali  ya Rufa ya Lindi, Diana Ngowi katika maojiano maalumu yaliyofanywa na BAGAMOYO KWANZA BLOG ambayo ilitaka kujua hali ya ukusanyaji wa Damu pamoja na matumizi yake katika Hospitali hiyo.

Ngowi alisema kwa kipindi cha miezi mitatu January-machi 2019 Hospitali hiyo ilikusanya jumla ya Lita 372 za damu huku akitaja matumizi ya Damu kwa mwezi lita 110.

Alisema 55% ya Damu inayotumika katika hospitali hiyo ni kwa ajili ya akinamama wajawazito 20% kwa ajili ya wagonjwa wa upasuaji, 10% watoto wachanga na asilimia 15 makundi mengine.

Ngowi alitaja sababu kubwa ya kundi hilo kuwa na mahitaji ya damu ni matatizo wakati wa kujifungua ambayo hupelekea upasuaji , kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua, mahudhurio hafifu ya Kliniki, kutotumia vidonge vya kuongeza damu vinavyotolewa katika Kliniki.

Nae Merina Bwago Mtaalamu wa Maabara wa Manispaa ya Lindi alisema kuwa licha ya kufanya uhamasishaji kupitia radio za kijamii zilizopo mkoani hapo pamoja na matangazo mbali mbali lakini bado jamii kubwa ya wananchi wanaoishi katika manispaa hiyo wamekuwa na tabia ya kuchangia damu kwa matukio mfano wakati wa kampeni au wanapokuwa na mgonjwa aliekuwa na mahitaji ya damu.

wambo alisema kuwa hali hiyo ya uchangiaji wa Damu inawafanya wakusanye kiasi kidogo cha damu inayotakiwa kutumika kama dharula kulingana na mahitaji ya damu yaliyopo katika hospital hiyo Mbwambo aliongeza kuwa watu wengi hawapendi kuchangia damu kwa kuhofia kupimwa magonjwa mbali mbali kama vile ukimwi, kaswende, manjano na magonjwa mengine ya zinaha

“lakini pia kuna baadhi ya vitu wanaviogopa Damu yako mpaka ije itumike imeshafanyiwa vipimo visivyopungua vinne , ugonjwa wa presha, kaswende, ugonjwa wa manjano ukimwi pamoja na wingi wa damu , sasa hivi vinne kidogo ni changamoto.

Watu wengi wanaona nikienda pale si nitagundulika nina ukimwi,si nitagundulika nina manjano bila kujua ukichangia damu kunafaida ya kujua hivyo vitu, na kuchangia damu hulipii hela yoyote lakini ukichangia unapimwa hivyo vipimo na ukibainika unaugojwa unapatiwa matibabu” alisema Bwambo.

Ugo amandusi na bakari juma ni miongoni mwa vijana wachache katika manispaa ya lindi ambao wamejiwekea utaratibu wa kuchangia Damu kila baada ya Miezi mitatu walisema kuwa kuchangia kwao damu kumekuwa kukiwasaidia pindi wanapokuwa na wagonjwa katika hospitali mbali mbali hapa nchini wanapokuwa na mahitaji ya damu hutumia kadi zao za uchangiaji na kuwawekea ndugu zao.

Ugo alisema ameamua kuchangia Damu ili kuwasaidi watu wenyemahitaji ya huduma hiyo huku akisema kuwa kutoa kwake damu ni sawa na sadaka kubwa kwa mwenyezimungu.

Nae Bakari Juma alitumia fursa hiyo kuwaasa wakazi wa Manispaa hiyo kujenga tabia ya kuchangia damu ili kuwasaidia watu wenye mahitaji ya Damu ikiwa ni  pamoja na kundi la akina mama wajawazito na watoto wadogo

No comments:

Post a Comment