Wednesday, June 26, 2019

SERIKALI PWANI YABAINI CHANGAMOTO 9 BIMA YA AFYA.

Image may contain: 1 person, standing
Na Omary Mngindo, Miono

SERIKALI imeeleza kuwa, imebaini maeneo tisa yaliyochangia kutofikiwa kwa malengo ya mfuko wa Bima ya afya CHF, iliyolenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya tiba, kwa wananchi.


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, amebainisha hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mji Mkuu, Kata ya Miono, Halmashauri ya Chalinze, wilayani Bagamoyo mkoani hapa, huku moja ya changamoto hiyo akiitaja kuwa ni mfumo.


Mkuu wa wilaya ya Mafia Shaibu Mnunduma yeye amemhakikishia Mhandisi Ndikilo kwamba, atawafikishia wakuu wenzake maagizo yote yliyotolewa ili kuboresha huduma, huku akiwataka wananchi kuchangamkia bima kwa ajili ya kujipatia huduma ya afya.


Mganga Mkuu mkoani Pwani Dkt. Gunini Kamba ameiambia hadhara hiyo kwamba, faida ya bima ya afya iliyoboreshwa, mojawapo ni mgonjwa kupata huduma ngazi za Kitongoji, Kijiji Wilaya mpaka Mkoa, tofauti na hapo awali.


Awali taarifa ya Halmashauri ya Chalinze ikisomwa na Mganga wa halmashauri hiyo Dkt. Rahimu Hangai, imeeleza kwamba vijiji 83 kati ya 84, tayari vimeshanunua simu, kwa ajili ya kuandikisha wananchi, ambao watanufaika na huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment