Saturday, June 29, 2019

KINA MAMA WAJAWAZITO 18 WAFANYIWA UPASUAJI KILWA.


 Chumba cha upasuaji katika kituo cha Afya Kilwa Msoko, wilayani Kilwa mkoa wa Lindi.

 
Jengo la kituo cha Afya Kilwa Msoko, wilayani Kilwa mkoa wa Lindi, Picha zote Na Hadija Hassan.
..................................

 NA HADIJA HASSAN, LINDI…


Jumla ya kina Mama wajawazito 18 kutoka katika kata ya masoko na maeneo jirani wamefanyiwa upasuaji mkubwa katika kituo cha afya cha kilwa masoko kilichopo katika Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi baada ya kukosa Huduma hiyo kwa miaka mingi.


Hayo yameelezwa na Mganga Mfawidhi wa kituo hicho cha Afya Dkt, Daud Selema jana alipokuwa akizungumza na BAGAMOYO KWANZA BLOG ilipotembelea kituoni hapo.


Dkt. Selema Alisema upasuaji huo ni wa miezi Saba kuanzia September 2018 mpaka April 2019.
Alisema kuwa kituo hicho cha Afya Masoko ni miongoni mwa vituo 44 vya Afya Nchini vilivyofanyiwa ukarabati na Serikali lengo likiwa kuzingatia majengo ya Muhimu katika utoaji wa huduma za Mama, Baba na Mtoto.


Aliongeza kuwa, kufuatia ukarabati huo kituo hicho cha Afya kimeshaanza kutoa huduma za upasuaji ambao ndio lengo kuu la vituo vinavyokarabatiwa ili kuweza kutoa huduma za dharula kwa kina Mama wajawazito wanaopata changamoto wakati wa kujifungua.


Alisema kabla ya kufanyiwa ukarabati huo walikuwa wanalazimika kumuhamisha Mama Mjamzito ambae ameshindwa kujifungua kwa njia ya kawaida na kumpeleka katika Hospital ya Wilaya ambayo ipo umbali wa kilometa 30 kutoka kituo hicho cha Afya kilipo.


“hali hii ilikuwa ni hatari kwa usalama wa uhai kwa Mama Mjamzito mwenyewe na hata kwa Mtoto atakae zaliwa kwani kutokana na muongozo wetu ni lazima mama huyo awe amefikia hatua Fulani ya uchungu na tuthibitishe kwamba kweli atashindwa kujifungua kwa kawaida ndipo tunaweza kuamua Mama huyo afanyiwe Upasuaji ambapo hata hivyo Huduma hiyo haikuwepo” Alifafanua Dkt, Selema.


Hata hivyo DKT, Selema aliwataka kinamama wajawazito kuwahi kituo cha Afya mapema pindi wanapojisikia dalili za uchungu ili watakapoanza kupata matatizo madogo madogo wakati wa kujifungua waweze kupatiwa huduma ya upasuaji mapema ili kumuokoa mama na mtoto atakae zaliwa.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti Baadhi ya kina Mama waliokuja kupatiwa Huduma za Matibabu Katika Kituo hicho cha Afya akiwemo Asha Kiambi Mkazi wa Mtaa wa Mifugo kilwa Masoko na Kibibi Duka Mkazi wa Kilwa Masoko Walisema kuwa kutolewa kwa huduma za upasuaji Katika Kituo hicho Cha Afya kumewasaidia kupungunza gharama za Usafiri pindi Mama mjamzito anapotakiwa kupewa Rufaa kwenda Hospital ya Wilaya.


"Hapo zamani Kama Mgonjwa wako atapewa Rufaa kwenda Katika Hospital ya Wilaya tulikuwa tunalazimika kuchangia Mafuta kwa ajili ya Gari ya kumbeba Mama huyo Mjamzito lakini kwa sasa tunaishukuru Serikali kwa kutuletea huduma za Upasuaji Katika Kituo Chetu ambapo gharama hizo sasa tutaondokana nazo"alieleza kiambi.


 "Uwepo wa Huduma hii pia umeturahisishia kupata muda wa ziada wa kuendelea Kufanya majukumu mengine kwa wakati Mfano Kama utapewa Rufaa ya kwenda kwenye Hospital ya Wilaya lazima itakubidi ukae huko mpaka mgonjwa wako atakapopata nafuu na kurudi nyumbani lakini Hapa kwa kuwa pamekuwa Karibu na nyumbani unaweza ukamuhudumia mgonjwa na Ukafanya na mambo Mengine kulingana na Hali ya Mgonjwa wako" aliongeza Duka

No comments:

Post a Comment