Sunday, June 16, 2019

WAKULIMA WA UFUTA LINDI WAONYWA.

Baadhi ya wakulima wa zao la Ufuta katika kijiji cha Namangale Halmashauri ya wilaya ya Lindi Mkoani Lindi wakishuhudia uendeshaji wa mnada wa zao hilo.
Mrajisi msaidizi wa Vyama vya Ushirika wa Mkoa Huo Robert Nsunza, akizungumza wakati wa mnada huo.
.................................
NA HADIJA HASSAN, LINDI.


SERIKALI mkoani Lindi imesema haitasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa kiongozi yeyote wa Chama Cha Msingi (AMCOS) atakaehujumu Mfumo wa uuzwaji wa zao la ufuta kwa Njia ya Mnada kwa kuchanganya zao hilo pamoja na Mchanga.


Hayo yamesema na Mrajisi msaidizi wa Vyama vya Ushirika wa Mkoa Huo Robert Nsunza June 15, 2019 katika Mnada wa zao hilo uliofanyika Ghara la Chama cha Msingi Namangale AMCOS katika kijiji cha Namangale Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Mkoani humo.


Nsunza alisema ili wakulima waendelee kupata bei mzuri katika zao hilo ni muhimu kwa watendaji katika Vyama vya Ushirika kuwa makikini katika Ufuta wanaoupokea kutoka kwa wakulima unakuwa kwenye ubora unaotakiwa.


“Serikali haitakuwa tayari kuona mnunuzi anakutana na Ufuta ambao utakuwa umechanganywa na mchanga , ndio maana tunawaambia viongozi katika vyama vyao kabla ya kuupokea Ufuta kutoka kwa mkulima na kuuingiza katika ghala ni lazima ufuta huo waumwage chini wajilidhishe ndio waupime”


Alisema Nsunza “Hatutakuwa tayaari kuona mtu anafanya hujuma yoyote katika hili, endapo mnunuzi atatoa taarifa kwamba amekuta mchanga ama takataka zozote katika Ufuta alioununua, viongozi wote wa chama husika Serikali itawawajibisha” Aliongeza Nsunza.


Nae Makamu Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika Lindi Mwambao kinachowaunganisha wakulima wa Wilaya za Lindi, kilwa na Manispaa ya Lindi Mkoani Humo Rashid Masudi aliwataka viongozi wa vyama vya Msingi wa chama hicho kuhalakisha maandalizi ya hesabu mara baada ya kukamilika kwa minada ili wakulima waweze kulipwa fedha zao kwa wakati.


Kwa upande wake Tadei Mbwago Mwenyekiti wa Namangale AMCOS alisema suala la kuuweka ufuta katika hali ya usafi ni jukumu la pande zote kuanzia kwa wakulima na wapokeaji hiyo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza ni vyema wakulima hao wakahakikisha ufuta wao unakuwa safi kabla ya kupeleka katika maghara kwa ajili ya kuupima ikiwa ni pamoja na kuupeta ili kuondoa majani na takataka zingine.


Akizungumza kwa niaba ya wakulima wengine Nuru Kambanga Mkazi wa kijiji hicho cha Namangale alisema anaishukuru Serikali kwa mfumo waliouweka wa kuuza zao hilo kwa njia ya mnaa kwani imewafanya wauze zao hilo kwa bei mzuri ukilinganisha na misimu iliyopita.


Katika Mnada huo wa Pili wa Chama kikuu cha Ushilika Lindi Mwambao jumla ya Makampuni 14 yaliomba kununua Ufuta huo ambapo Kampuni 6 kati ya hizo ndio yalifanikiwa kununua zao hilo kwa bei ya Juu ya Tsh. 2953/= na bei ya Chini 2905 ambapo jumla ya Tani 3220 na kilo 235 ziliuzwa
  
Baadhi ya wakulima wa zao la Ufuta katika kijiji cha Namangale Halmashauri ya wilaya ya Lindi Mkoani Lindi wakishuhudia uendeshaji wa mnada wa zao hilo.
 

No comments:

Post a Comment