Monday, June 24, 2019

ZAIDI YA TANI 5,000 ZA UFUTA ZAUZWA MKOANI LINDI.

Sehemu ya magunia ya zao la ufuta kama yanavyoonekana pichani wakati wa mnada uliofanyioka mkoani Lindi.
....................................................

 NA HADIJA HASSAN, LINDI.


Jumla ya Tani 5405 na kilo 791 za ufuta wa wakulima wa Chama kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao kinachojumuisha wakulima wa Wilaya za Lindi, Kilwa na Manispaa ya Lindi Mkoani humo zimeuzwa Katika Mnada wa Tatu wa zao hilo kwa Bei ya Juu ya Tsh. 2802 na Bei ya chini 2738.


Mnada huo wa Tatu umefanyika Katika ghara la chama cha Msingi Mnazi mmoja AMCOS kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ambapo Jumla ya Makampuni 14 yaliomba kununua ufuta huo.


Akizungumza Mara baada ya kufanyika mnada huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Jomari Satura pamoja na mambo Mengine aliwaasa wananchi wa Lindi kwa ujumla kutumia fedha wanazozipata Katika mauzo ya ufuta kuwekeza Katika mambo ya kimaendele.


Alisema ili kilimo hicho kiweze kuonekana kimeleta tija Katika Mkoa huo ni vyama, wakulima baada ya kupata fedha zao wakafanya mambo yanayoweza kuwainua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba mzuri ambayo itaonyesha utofauti wa kabla ya Msimu na baada ya msimu


 Aliongeza kwa kusema kuwa, ni ajabu kuona mpaka Msimu wa mauzo unaisha Huku mabilioni ya fedha yakiwa yamewafikia wananchi lakini maendeleo ya Moja kwa Moja yasionekane.


Nae Mstahiki meya wa Manispaa Lindi Lidume Liumbo Akifunga mkutano huo wa Mnada wa ufuta Alitumia fulsa hiyo kuwaasa wananchi wa Manispaa hiyo kuongeza Tija ya uzalishaji wa zao hilo Ili kuweza kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja, Mkoa na nchi kwa ujumla.

Wananchi wakiwa katika mnada wa Ufuta mkoani Lindi.

No comments:

Post a Comment