Sunday, June 16, 2019

BODI YA KOROSHO YATAKA WAKULIMA KUJISAJILI KWENYE DAFTARI LA WAKULIMA.

NA HADIJA HASSAN, LINDI.

BODI ya Kaorosho Tanzania imewataka wakulima wa zao hilo kujitokeza kwa wingi kujisajili kwenye Dafutari la kudumu la wakulima ili kupata taarifa sahihi za wakulima wa zao hilo kwa lengo la kujua maeneo halisi ya wakulima pamoja na mahitaji yao.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania Francis Alfred alipokuwa akitoa salamu za bodi hiyo katika uzinduzi wa mafunzo ya Matumizi ya Viuwatilifu yaliyofanyika katika kata ya Maumbika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani Humo.

Alfred alisema usajili huo utawasaidia wao kama serikali kufahamu maeneo halisi ya wakulima kuanzia anapoishi na eneo la shamba la mkulima ikiwa ni pamoja na kufahamu mahitaji ya pembejeo za wakulima katika eneo husika.

Alisema bodi ya korosho imeshasambaza wataalamu wa bodi hiyo kwenye wilaya zote Nchi mzima ambazo zinalima zao hilo ili waongeze nguvunya kwa wataalamu ambao wapo wilayani wanaohusika na ukusanyaji wa fomu hizo za usajili lengo likiwa ni kukamilisha usajili huo ifukapo june 20 mwaka huu wa 2019.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Huo Godfrey Zambi alisema kuwa usajili huo licha ya kumtambua mkulima lakini pia Mkulima huyo ataweza kupatiwa kitambulisho kitakachomuwezesha kupata mkopo katika taasisi mbali mbali za kifedha.

Alisema jambo la usajili kwa wakulima ni muhimu kufanyika Kwani itawasaidia Serikali kuondokana na adha ya kuhakiki wakulima hao Mara baada ya kupeleka mazao hayo kwenye maghara kwa ajili ya mauzo pamoja na kutambua mahitaji halisi ya pembejeo za wakulima wa zao hilo na mahitaji Mengine Kama vile Miche na mbegu za mikorosho.

Ndemanga aliongeza Kuwa usajili huo pia utaisaidia Serikali kuzuia mianya ya wafanya biashara wanaowanyonya wakulima wanaonunua zao hilo kwa njia ya choma choma (kangomba).

Hata hivyo Ndemanga alitumia nafasi hiyo kukanusha juu ya uvumi unaoenezwa na baadhi ya wananchi kuhusisha usajili huo na utozwaji wa kodi kwa wakulima kuwa sio kweli, na kubainisha kuwa lengo lengo la usajili huo ni kupata taarifa za wakulima zilizo sahihi ili Serikali ijue namna ya kuwasaidia na kuwapa huduma

No comments:

Post a Comment