Saturday, June 29, 2019

RUVUMA YAFANIKIWA KUTOA CHANJO KWA WATOTO WACHANGA KWA ASILIMIA 102

Dk.Jair Khanga Mganga mkuu Ruvuma
  Joyce Joliga  Songea.
Wazazi wameshauliwa kuacha  utoro wa kuwapeleka watoto wao Kliniki ili waweze kupata chanjo za kuwakinga na Ulemavu au vifo  vinavyotokana na maradhi mbalimbali .
  Hata hivyokwa mujibu wa  takwimu za mwaka 2017 za  Shirika la afya duniani (WHO)zinaonyesha kuwa upatikanaji wa chajo umeongezeka ambapo watoto 85% wanachanjwa  ambapo zaidi ya watoto 16 walipata chanjo muhimu tatu za kuwakinga dhidi ya magonjwa ya kuambukiza ambayo wakati mwingine usababisha ulemavu.
Tayari  Mkoa wa Ruvuma imefanikiwa kutoa chanjo  ya Matone Polio,kifua kikuu kwa watoto weny e umri chini ya miaka mitano kwa 102% katika kipindi cha January-Machi 2019 .
 Mganga mkuu mkoa wa Ruvuma Dkt.Jair Khanga anasema hali ya utoaji chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano inazidi kuhimarika ambapo  kwa mwaka 2018  asilimia 93 walipata chanjo hizo na kutokana na mikakati mbalimbali waliyojiwekea  idadi ya watoto waliopata kinga imepanda  na wanatarajia kufikia 130% hadi kufikia Desemba 2019.

Anasema, Chanjo hukinga maradhi, ulemavu na vifo vitokanavyo na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ikiwa ni pamoja na surua, homa ya ini (hepatitisi B), dondakoo, kifaduro, nimonia, polio, kuhara kunakosababishwa na virusi vya rota, rubela na pepopunda.
Dkt.Khanga anasema, Watoto waliopata chanjo huwa wamekingwa dhidi ya magonjwa haya hatari, ambayo kwa kawaida huweza kusababisha ulemavu au kifo.

Anasema ,elimu iliyotolewa kwenye  kampeni maalum iliyoanzishwa ya kuwaelimisha wazazi umuhimu wa chanjo kwa watoto imesaidia wazazi na walezi kupata uelewa  na kuwapeleka watoto kupata chanjo  hali ambayo imesaidia kuongezeka kwa  idadi ya waliopata chanjo hivyo kuwanusuru na magonjwa bali mbali ikiwemo  upofu, ulemavu pamoja na vifo.

Dkt.Khanga anaeleza kuwa elimu inaendelewa kutolewa kwa jamii huduma za mkoba pia chanjo  zinapatikana kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya , hospitalini  pia commitment ya wahudumu ni kubwa wanahakikisha  kila mtoto anafikiwa.
Aidha, ameongeza kuwa ni asilimia ya wanawake 82.2% pekee ndio wanajifungulia hospitalini , kwenye vituo vya afya na Zahanati  na asilimia 17.8%  wanajifungulia  majumbani na kwa wakunga wa jadi  hivyo hakuna  chanjo wanazopata na amewashauri kujifungulia  Hospitali ili watoto wao waweze kupata chanjo  hizo muhimu  .
Amewashauri wazazi na walezi wa watoto wenye umri kuanzia  0- 5 miaka kuhakikisha wanawapeleka watoto wao kliniki na kufata maelekezo yote wanayopewa na wataalam wa afya ili kuweza kuwa na jamii yenye afya bora  na salama .
 kwa upande wake Mariam  Ally Mkazi  Kijiji cha Lyangweni amekiri kuwepo kwa uzembe wa baadhi ya wazazi kutowapeleka watoto wao  kliniki ambapo amesema wapo ambao wanaamini madawa ya kienyeji  kuwa yanawakinga watoto wao na wapo ambao wanapuuza tu  na hawana sababu ya msingi.
“kiukweli hata mimi sikujua kama kuna umuhimu wa watoto wetu kupelekwa  Kliniki , kutokana na kubanwa na kazi nyingi za kilimo  nimekuwa mzembe naahidi kuanzia sasa nitampeleka mwanangu  Husein kliniki ili niweze kumnusuru na magonjwa mbalimbali,”alisema

No comments:

Post a Comment