Sunday, June 30, 2019

CCM WILAYA YA MKURANGA YAANZA ZIARA.

Na Omary Mngindo, Mkuranga.

SEKRETARIET ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, ipo katika ziara ya kikazi kwenye Kata 25, lengo likiwa ni kujenga mahusiano zaidi na yenye tija, ndani ya chama hicho.


Katibu wa Sekretariet hiyo Hanzuruni Mtebwa ameiambia BAGAMOYO KWANZA BLOG kwa njia ya simu kwamba, ziara hiyo chini ya Katibu wa chama hicho wilaya Rukia Mbasha aliyehamia wilayani humo hivi karibuni akitokea mkoani Lindi, inalenga kujenga mahusiano ya wana-CCM hao.


Ametanabaisha kuwa, tayari wameshazitembelea Kata saba kati 25, ambazo ni Tengelea, Vianzi, Vikindu, Mwandege, Mkuranga, Mtambani na Mipeko ambapo pia ziara hiyo imetumika kumtambulisha Katibu huyo mpya.


Aidha katika kufikia malengo hayo, Sekretariet hiyo imekabidhi REJA za wanachama kwa Mabalozi wote wenye jukumu la balozi, ili kuhakiksha wanaweka taarifa sahihi za wanachama wanaoishi ndani ya eneo lao la uongozi.


"Sanjali na hayo, pia tumewahimiza kuwa na vikao ikiwemo kuanza maandalizi ya uchaguzi ujao kuanzia serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, kama unavyofahamu mwishoni kwa mwaka huu tutaanza kuchagua Wenyeviti," alisema Mtebwa.


Sanjali na hayo, Sekretariet hiyo imempongeza Mbunge wao Abdallah Ulega, ambaye ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, kwa namna anavyojitoa katika kukitumikia chama na wananchi, ambapo ameboresha jengo la sanjali na kuweka fremu za biadhara ikiwa ni mradi wa chama hicho.


"Katika ziara hiyo tumepokea ushuhuda kutoka kwa viongozi, waasisi na wanachama wa CCM, juu ya jitihada za kukisaidia Chama kwa kuchangia Ujenzi wa majengo ya Chama ambapo Mbunge Abdallah Ulega amejitoa katika hilo," alisema Mtebwa.


Akizungumzia usajili wa wanachama kwa mfumo wa Kielekrtonic, Katibu huyo alisema kuwa katika uzinduzi uliofanyika kila Kata, wanachama zaidi ya 100 wamasajiliwa, huku akigusia changamoto ya uchache wa simu ambapo kila eneo kuna simu moja tu.


Kutokana na hali hiyo, Sektretariet imeanzisha harambee iliyokusanya kiasi cha zaidi ya shilingi milioni tano, ikiwemo ahadi pamoja na pesa taslim zitakazotumika kwa ununuzi wa simu ili kuboresha usajili kwa wana-CCM hao.

No comments:

Post a Comment