Sunday, June 2, 2019

DC BAGAMOYO ATOA NASAHA KWA WANANCHI.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawa  amefuturisha ofisini kwake na kuwataka wananchi kudumisha amani iliyopo wilayani humo ili kila mmoja afanye shughuli zake za maendeleo kwa uhuru.


Alisema katika kipindi hiki cha Mwezi wa Ramadhani kila mmoja amejifunza subira, huruma na kusamehe na kusema kuwa hali hizo zinapaswa ziendlezwe katika miezi mingine iliyobaki.


Katika hutuba yake mara baada kufuturu aliwataka wananchi wa wilaya ya Bagamoyo kujitokeza kwenye uchaguzi wa serikali za mita unaotarajiwa kufanyika mwaka huu ili kila mmoja ashiriki kwa nafasi yake kuchagua viongozi watakaoleta maendeleo ndani ya wilaya hiyo.


Alisema wale wote wenye sifa wajitokeze kugombea nafasi hizo huku wananchi wote wanapaswa kushiriki kwenye uchaguzi huo kwa kujitokeza kupiga kura.


Aidha, alisema takwimu inaonyesha Mkoa wa pwani unaongoza kwa ujenzi wa viwanda hapa nchini na kwamba wilaya ya Bagamoyo ni miongoni mwa wilaya zenye viwanda vingi mkoani Pwani.


Alitumia nafasi hiyo kuwataka wazazi na walezi kuendelea kuwasimamia watoto waende shule ili hatimae wapate elimu itakayowasidia kupata ajira kwenye viwanda hivyo.


Mkuu huyo wa wilaya amemalizia kwa kuwataka wanachi wa Bagamoyo kujiandaa kuupokea mwenge wa uhuru ambao unatarajiwa kuingia katika wilaya hiyo Tarehe 24 Julai.


Alisema Bagamoyo imekuwa ikifanya vizuri kila mwaka katika mapokezi ya Mwenge na kwamba kufanya vizuri huko kunatokana na umoja, mshikamano miongoni mwa wananchi na wataalamu kutoka idra mbalimbali za serikali na watu binafsi.


Aliwataka wananchi kuendelea na mshikamano huo ili kwa mara nyingine wilaya ya Bagamoyo ifanye vizuri katika miradi yake ambayo inatarajiwa kuzinduliwa na Mbio za Mwenge za mwaka 2019.


 Katibu wa ccm wilaya ya Bagamoyo, Salim Mtelela wa kwanza kushoto, akiwa na mzee maarufu mjini Bagamoyo Aliy bin Nasiri (katikati na Sheikh Ramiya Muhammad Ramiay, kulia.

 Waislamu an wanachi mbalimbali wakiwa katika mstari wa kupata futari ofisini kwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo alipokuwa anafuturisha katika viwanja vya ofisi yake.

 
Waislamu an wanachi mbalimbali wakiwa katika mstari wa kupata futari ofisini kwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo alipokuwa anafuturisha katika viwanja vya ofisi yake.



No comments:

Post a Comment