Thursday, June 13, 2019

SERIKALI KUENDELEA KUTUMIA LUGHAA MBILI ZA KUFUNDISHIA.

Image may contain: 1 person, sitting
Wazari wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema suala la lugha ya kufundishia na kujifunzia ni la kisera kama iliyotamkwa katika Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014.


Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo Bungeni ambapo amesema Sera hiyo imebainisha matumizi ya lugha mbili za Kiswahili na Kiingereza ambapo lugha ya Kiswahili inatumika kufundishia katika ngazi ya Elimu ya Awali na Msingi, Vyuo vya Ualimu ngazi ya Cheti na Vyuo vya Ufundi Stadi wakati lugha ya Kiingereza inatumika katika ngazi za Elimu ya Sekondari, Vyuo vya Kati ba Vyuo Vikuu.


"Hii ni kwa sababu ya umuhimu wa lugha hiyo katika masuala ya Kitafa, Kikanda na Kimataifa kwa mawasiliano na biashara ili kuwajengea wanafunzi ufahamu na umahiri ktk lugha hiyo," amesisitiza Prof. Ndalichako.


Waziri Ndalichako amesema Kutokana na umuhimu wa lugha ya Kiingereza serikali itaendelea kutumia lugha mbili katika kufundishia pamoja na kuimarisha matumizi ya lugha ya kiswahili ili Watanzania wengi zaidi kunufaika na fursa zinazojitokeza nje ya nchi.


Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaangalia utaratibu wa kutumia Vyuo vilivyopo kuandaa walimu wanaofundisha shule za English Media nakuendelea kukitangaza kiswahili ikiwa ni pamoja na kutumika ktk mikutano ya Afrika mashariki na kufundishwa nje ya nchi.


No comments:

Post a Comment