Monday, June 24, 2019

DC. BAGAMOYO AZINDUA SOKO LA WANAWAKE WAJASIRIAMALI.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, (katikati) akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake wajasiriamali wilayani humo, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis, (wa pili kulia) akipunga mkono mara baada ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Zainabu Kawawa (kushoto) kukata utepe kama ishara ya kuzinduliwa rasmi kwa soko la pamoja la wanawake wajasiriamali Bagamoyo.
.........................................

 Na Selestian James

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa  amezindua soko la Pamoja la wanawake wajasiriamali wilayani humo, ikiwa kama hatua ya kuwakwamua katika shughuli zao za kiuchumi.


Shuguli hiyo ya uzinduzi iliyofanyika hivi karibuni katika mgahawa wa smoke house uliopo kata ya Dunda wilayani Bagamoyo ilikutanisha wanawake wajasiriamali kutoka kata mbalimbali wilayani humo ikiwemo kata ya Dunda, Magomeni, Zinga, Kiromo na Nianjema.


Wanawake hao walifika wakiwa na bidhaa mbalimbali za ubunifu na mazao mbalimbali ya kilimo zikiwa kama shughuli kuu za kujiingizia kipato.


Aidha Mkuu huyo wa wilaya amewapongeza wanawake hao kwa hatua ya kuanzisha soko hilo kwa kutumia eneo lao binafsi badala ya kuisubiri serikali.


Alisema amefarijika na hatua hiyo na kwambaametoa ahadi ya kushirikiana nao bega kwa bega kuhakikisha wanapata  eneo kubwa zaidi kwa ajili ya ujenzi wa soko.


Alitumia nafasi hiyo kuwataka viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi  wilayani humo kushirikiana nae na kumuonesha ni sehemu gani inayofaa kulingana na shughuli zao, ili nae kama kama kiongozi wa serikali afuate taratibu atimae wafanikishe.


"Hatuwezi kuwa na bidhaa nzuri kama hizi halafu tukakosa soko la kuuzia, bihaa nzuri kama hizi ndio alama ya Bagamoyo" Alisema Zainabu.


lakini pia kiongozi huyo amewakaribisha ofisini kwake kinamama hao ambapo kila siku za jumanne huwa anasikliza kero mbalimbali za wananchi na kuona ni namna gani anaweza kuzitatua akiwa na wataalam mbalimbali wakiwemo wanasheria.


Naye mweyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanaweke Kiuchumi wilaya ya Bagamoyo, Teddy Devis alimshukuru mkuu wa wilaya huyo kwa kuweza kufika eneo hilo  kuwatia moyo  na kuwaunga mkono.


Alisema kwa muda mrefu wamekosa sehemu ya kuwaunganisha  kama wanawake wajasiriamali, ambapo sasa kupitia soko  hilo litakalokua linafanyika kila siku ya jumamosi litawafungulia fursa kuweza kuuza na kutangaza bidhaa zao ndani na nje ya nchi.


kwa upande wa wanawake waliokuwepo katika eneo hilo wameonesha furaha zao kwa hatua hiyo iliyochukuliwa na kiongozi huyo.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, akiwa anaangalia bidhaa za wajasiriamali katika uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.
 
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, pamoja na Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis, wakifurahia jambo wakati akitembelea bidhaa za wajasiriamali kwenye uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.
 
Viongozi mbalimbali wa chama na serikali waliofika kushuhudia uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.

PICHA ZOTE NA SELESTIAN JAMES. 
    

No comments:

Post a Comment