Posts

WANANCHI 10,378 WAFIKIWA NA HUDUMA YA AFYA YA MACHO LINDI.

Image
NA HADIJA OMARY, LINDI. Jumla ya Wananchi 10,378 kutoka halmashauri sita za Mkoa wa  Lindi  wamefikiwa na huduma ya Afya ya macho ambapo kati yao 9690 wamefanyiwa vipimo na kupatiwa matibabu  Hayo yameelezwa na Dokta Sharifu Hamza kwa niaba ya Mganga Mfawidi wa hospital ya Rufaa MKoa wa Lindi Sokoine, Jana oktoba 10 wakati wa maadhimisho ya Afya ya macho yaliyofanyika kimkoa Katika hospital hiyo ya Rufaa Sokoine huko Manispaa ya Lindi . Zoezi hilo la utoaji Elimu ya Afya ya macho sambamba na vipimo na matibabu limeendeshwa kwa ufadhili wa mashirika ya  Heart to Heart foundation,  CBM pamoja na Korea church . Amesema  zoezi hilo lililoendeshwa kwa siku saba kuanzia oktoba 4 hadi 10 wataalamu walipita katika shule mbalimbali kwa halmashauri zote sita kutoa elimu pamoja na kutoa matibabu kwa wananchi walioonekana na changamoto ya afya ya macho. maadhimisho hayo ya Afya ya macho  yanayohimiza vijana na watoto kupenda macho yao na  kuitaka dunia kuonge...

WAANDIKISHAJI WAPIGA KURA NACHINGWEA, WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

Image
  Na Hadija Omary, Lindi. Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi Mhandisi chionda kawawa ametoa Rai kwa Waandikishaji wa wapiga Kura kuzingatia kanuni za uchaguzi wakati wa zoezi hilo linalotarajia kuanza oktoba 11 hadi 20 mwaka 2024 Chionda ametoa Rai hiyo alipokuwa anazungumza wakati wa Mafunzo kwa Waandikishaji wapiga Kura kutoka Katika vitongoji vyote vya halmashauri hiyo yaliyofanyika Katika ukumbi wa TTC Wilayani Nachingwea  Katika mafunzo hayo Jumla ya Waandikishaji 525 walipatiwa Mafunzo ambapo Kati ya hao 15 ni Waandikishaji wa akiba huku 36 wakiwa ni wasimamizi wa Uchaguzi Katika Ngazi ya Kata  Waandikkshaji hao wameapa mbele ya hakimu wa Wilaya Nachingwea na wako tayari kwa kuanza zoezi la uandikishaji,  Aidha, Mhandisi Chionda amewapongeza waandikishaji hao kwa kuteuliwa kufanya kazi hiyo na kuwaahidi kuwapa ushirikiano pale watakapohitaji, pia amewataka kufanya kazi kwa juhudi ili kufikia malengo na kufanya wananchi wengi kushiriki ku...

WAJASIRIAMALI WANAWAKE BUKOBA WAPATIWA ELIMU.

Image
  Na Alodia Dominick, Bukoba Wanawake wajasiriamali katika mji wa Bukoba wamepata elimu ya ujasiriamali, na kutakiwa kujiamini, kujithamini, kujiheshimu na kutojikweza. Mafunzo hayo yametolewa na kampuni ya Stein Group inayojihusisha na shughuli za kijamii na  mafunzo hayo yamefanyika Octoba 06, 2024 katika manispaa ya Bukoba. Meneja wa  Kampuni ya Stein Group mkoa wa Kagera Exavery Kyatwa ametaja lengo la kutoa mafunzo hayo kuwa ni kuwaelimisha wanawake wajasiriamali waliopo Manispaa ya Bukoba ili watoke hatua moja na  kwenda hatua nyingine kwa kujiendeleza kiuchumi. Naye Mkurugenzi wa taasisi hiyo Taifa Mayamba Mbilinyi amesema, wameanza na wajasiriamali wa manispaa ya Bukoba yenye kata 14 na wajasiriamali wanawake wapatao 200 na baadaye wanatarajia kuwafikia zaidi ya wajasiriamali 1,000 katika wilaya nyingine za mkoa wa Kagera kwa kutoa elimu ya ujasiriamali. “Sisi tumelenga akina mama ili tuwajengee uwezo wa kujiamini katika kufanya biashara zenu, msiendelee kuwa...

DC MWANZIVA NSSF: LINDI ONGEZENI KUTOA ELIMU KWA WANACHI UMUHIMU WA KUJIUNGA NA MFUKO NA FAIDA ZAKE

Image
  Na Hadija Omary, LINDI. MKUU wa Wilaya ya Lindi Mkoani Humo Bi.Victoria Mwanziva  amewataka watumishi WA Mfuko wa hifazadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Lindi kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi wengi juu ya Umuhimu wa kujiunga na mfuko huo na faida zake Mwanziva ametoa Rai hiyo oktoba 07/2024 wakati akizungumza na watumishi na wanachama wa Mfuko huo wa NSSF Mkoa wa Lindi Katika uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika huko manispaa ya Lindi . Mwanziva Amesema wakati huu ambao Mfuko umeboresha mfumo wa sekta isiyo rasmi kwa wanachama waliojiajiri na kuandaa skimu maalumu kwa wafanyakazi walio Katika sekta rasmi ili kuweza kuchangia kwa hiari kupitia skimu hiyo ya (NISS NA SS)  pamoja na mambo mengine zinalenga kupanua wigo wa huduma za hifadhi ya Jamii hivyo ni wajibu wao kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi . Mifuko hii ya Watu kujichangia wenyewe ebu twendeni tukaongeze Elimu kwani tuna wananchi wengi Sana ambao wamejiajiri wafanyabiashara, wajasiriamali tuweke mpang...

WAZEE WAASWA KUWA MBELE KATIKA KUHAMASISHA USHIRIKI WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Image
  NA HADIJA OMARY, LINDI. Wazee wa Nachingwea wameaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vijiji unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba mwaka huu 2024. Wito huo  umetolewa na Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Nachingwea Robert Mmari alipokuwa akizungumza na wazee maarufu wa Wilaya hiyo ambapo amesisitiza   kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na msaada wa wazee utahakikisha zoezi linafanikiwa Afisa Uchaguzi (W) ya Nachingwea ndugu Robert Mmari pia ameeleza kuwa sifa za mgombea na mpiga kura zimesha ainishwa, kwamba Mpiga kura lazima awe na akili timamu, awe na umri wa miaka 18 au zaidi, na awe mkazi wa kitongoji husika Wananchi wote wanatakiwa kupiga kura kwenye vitongoji walivyojiandikisha, huku zoezi la kuchukua fomu za kugombea likipangwa kuanza Novemba 1 Aidha, Msaidizi wa uchaguzi Joshua mnyang'ali Amesema kuwa kwa mwananchi  kushindwa kujiandikisha  kwa wakati uliopangwa, atapoteza h...

BASHE AWAHAKIKISHIA WAKULIMA WA KOROSHO KUPATA BEI NZURI

Image
  NA HADIJA OMARY,  LINDI. Waziri wa kilimo Hussain Bashe Amewahakikishia wakulima wa korosho kuwepo kwa bei nzuri ya zao Hilo Katika msimu wa mauzo 2024/2025 unaotarajiwa kuanza November 11 mwaka huu Waziri Bashe ameyasema  hayo  November 02, 2024 akiwa Mkoani Lindi wakati anazungumza na Wadau wa kilimo ambapo Amesema kuwa kutokana  na mfumo rafiki unaotumika Katika uuzaji wa mazao wa Soko la Bidhaa (TMX) Hana Shaka kuwepo kwa bei zinazoridhisha Katika minada " Tunaamini mwaka huu bei za korosho zitakuwa nzuri na kwa mara ya kwanza kwenye mfumo huu wa TMX tumeona makampuni ya kigeni ambayo yamejaribu kununua na zimepokea mzigo kama walivyotaka" ''Yaan wameshiriki wameiona katalog wameomba na kununua wakiwa huko huko nje na wameweza kupokea sasa maana yake   hamu imekuwa kubwa wanaweza kuuamini mfumo" Hata hivyo Bashe ameviagiza Vyama vikuu vya ushirika Mkoa wa Lindi kufanya utambuzi wa maghara ya kuhifadhia korosho kabla ya msimu mpya wa mauzo ya zao ...

MAAFISA KILIMO KATA KARAGWE WAPATIWA PIKIPIKI.

Image
  Na Alodia Dominick, Karagwe Halmashauri ya wilaya ya Karagwe mkoani Kagera yenye maafisa kilimo wa kata wapatao 33 tayari wote wamepatiwa usafiri wa pikipiki kutoka Wizara ya kilimo ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ubora. Maafisa kilimo hao wamepatiwa pikipiki kwa nyakati tofauti na Oktoba mosi, mwaka huu maafisa kilimo wapatao tisa ambao wameajiriwa hivi karibuni wamepatiwa pikipiki kama mwendelezo wa maafisa kilimo 24 ambao walitangulia kupata pikipiki hizo. Akizungumza katika halfa hiyo ya makabidhiano Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe Happiness Msanga ameishukuru serikali kupitia Wizara ya kilimo kwa kuendelea kuwakumbuka watumishi wa wilaya ya Karagwe hususani maafisa kilimo ngazi ya kata ambao shughuli zao kwa kiasi kikubwa zinategemea usafiri kutokana na ukubwa wa maeneo na umbali ili kuwafikia wananchi kwa wakati. "Nichukue nafasi hii kuwasisitiza maofisa wote ambao mmekabidhiwa pikipiki kwa ajili ya kufanikisha kazi zenu mzitunze na kuzitumia k...