BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI

 

BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba 2026. 



Bei ya petroli imeshuka kwa Shilingi 102 kwa lita, huku bei ya dizeli ikishuka kwa Shilingi 101 kwa lita. Bei hizo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 2 Septemba 2026, saa 6:01 usiku.


EWURA inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia, ambapo mabadiliko ya bei yanaendelea kuathiriwa pamoja na mambo mengine na hali ya kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati.


Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015, bei za mafuta zinaendelea kupangwa kwa kuzingatia mfumo wa soko.



Wafanyabiashara wote wa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zisizozidi bei elekezi, na wananchi wanashauriwa kutoa taarifa EWURA kwa kituo chochote cha mafuta kitakachouza zaidi ya bei elekezi.


Comments

Popular posts from this blog

RAIS DKT. SAMIA AKIWA PAMOJA NA MAKAMU WA RAIS DEOGRATIUS NDEJEMBI.

WATUMISHI WA AFYA KAGERA WAFANYA ZOEZI LA UTAYARI KUKABILIANA NA EBOLA

MWENGE WA UHURU, WAZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI YA MILIONI 900. BUKOBA

MAKAMU WA RAIS, ATEMBELEA OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA

MAKAMU WA RAIS AWASALIMU WANANCHI WA CHAMWINO

GLOBAL YASAFIRISHA KUNDI LINGINE LA WANAFUNZI KWENDA NJE YA NCHI.

OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA, YAMPONGEZA NDEJEMBI.