Sunday, October 6, 2024

WAZEE WAASWA KUWA MBELE KATIKA KUHAMASISHA USHIRIKI WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

 




NA HADIJA OMARY, LINDI.


Wazee wa Nachingwea wameaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vijiji unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba mwaka huu 2024.


Wito huo  umetolewa na Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Nachingwea Robert Mmari alipokuwa akizungumza na wazee maarufu wa Wilaya hiyo ambapo amesisitiza   kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na msaada wa wazee utahakikisha zoezi linafanikiwa



Afisa Uchaguzi (W) ya Nachingwea ndugu Robert Mmari pia ameeleza kuwa sifa za mgombea na mpiga kura zimesha ainishwa, kwamba Mpiga kura lazima awe na akili timamu, awe na umri wa miaka 18 au zaidi, na awe mkazi wa kitongoji husika Wananchi wote wanatakiwa kupiga kura kwenye vitongoji walivyojiandikisha, huku zoezi la kuchukua fomu za kugombea likipangwa kuanza Novemba 1


Aidha, Msaidizi wa uchaguzi Joshua mnyang'ali Amesema kuwa kwa mwananchi  kushindwa kujiandikisha  kwa wakati uliopangwa, atapoteza haki ya kupiga kura 


Hata hivyo Alisisitiza kuwa Halmashauri imejipanga vyema kuhakikisha wananchi wanapata elimu kuhusu uchaguzi na umuhimu wa kushiriki katika zoezi hilo


Kwa upande wake, Chief Nakotyo alibainisha kuwa kutakuwa na tukio maalum lenye ujumbe kuhusu maadili na hamasa ya uchaguzi litakalofanyika tarehe 7 na 8 Novemba na aliwataka wazee kuendelea kuhamasisha wananchi ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa mafanikio Vilevile, Joyce Chipanda, mkazi wa Kilimani Road, amewaasa wananchi kutopotosha wenzao na badala yake kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kulinda usalama na amani ya nchi


No comments:

Post a Comment