SUBIRA MGALU AULIZA HATUA YA FIDIA KWA WANANCHI WA BARABARA YA MAKOFIA–MLANDIZI

 

SUBIRA MGALU AULIZA HATUA YA FIDIA KWA WANANCHI WA BARABARA YA MAKOFIA–MLANDIZI



Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. CPA Subira Khamis Mgalu, ameuliza Serikali kuhusu hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya kuwalipa fidia wananchi wanaopitiwa na mradi wa Barabara ya Makofia–Mlandizi katika Kata ya Yombo.


Akitoa swali la nyongeza, Mhe. Subira amesema barabara hiyo imefungamanishwa na mpango wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na eneo la viwanda la Kwara, hivyo umuhimu wake unaendelea kuongezeka.


Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema kuwa Wizara tayari imekamilisha tathmini ya fidia na imewasilisha mahitaji hayo katika Wizara ya Fedha.


Amesema Serikali inaendelea na taratibu za kupata fedha, na mara fedha zitakapopatikana, wananchi waliostahili watalipwa fidia ili hatua za ujenzi wa barabara hiyo ziweze kuendelea.


Comments

Popular posts from this blog

RAIS DKT. SAMIA AKIWA PAMOJA NA MAKAMU WA RAIS DEOGRATIUS NDEJEMBI.

MWENGE WA UHURU, WAZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI YA MILIONI 900. BUKOBA

MAKAMU WA RAIS, ATEMBELEA OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA

TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA

MAKAMU WA RAIS AWASALIMU WANANCHI WA CHAMWINO

GLOBAL YASAFIRISHA KUNDI LINGINE LA WANAFUNZI KWENDA NJE YA NCHI.

OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA, YAMPONGEZA NDEJEMBI.