Tuesday, October 8, 2024

WAANDIKISHAJI WAPIGA KURA NACHINGWEA, WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

 



Na Hadija Omary, Lindi.


Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi Mhandisi chionda kawawa ametoa Rai kwa Waandikishaji wa wapiga Kura kuzingatia kanuni za uchaguzi wakati wa zoezi hilo linalotarajia kuanza oktoba 11 hadi 20 mwaka 2024


Chionda ametoa Rai hiyo alipokuwa anazungumza wakati wa Mafunzo kwa Waandikishaji wapiga Kura kutoka Katika vitongoji vyote vya halmashauri hiyo yaliyofanyika Katika ukumbi wa TTC Wilayani Nachingwea 



Katika mafunzo hayo Jumla ya Waandikishaji 525 walipatiwa Mafunzo ambapo Kati ya hao 15 ni Waandikishaji wa akiba huku 36 wakiwa ni wasimamizi wa Uchaguzi Katika Ngazi ya Kata 



Waandikkshaji hao wameapa mbele ya hakimu wa Wilaya Nachingwea na wako tayari kwa kuanza zoezi la uandikishaji, 



Aidha, Mhandisi Chionda amewapongeza waandikishaji hao kwa kuteuliwa kufanya kazi hiyo na kuwaahidi kuwapa ushirikiano pale watakapohitaji, pia amewataka kufanya kazi kwa juhudi ili kufikia malengo na kufanya wananchi wengi kushiriki kupiga kura siku ya tarehe 27 Novemba 2024.



Afisa Uchaguzi ndugu Robert Mmari amewasihi waandikishaji hao kufuata kuzingatia mambo mbalimbali waliyofundishwa na kuuliza pale wanapokosa majibu na sio kufanya kwa utashi.


"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"


No comments:

Post a Comment