Friday, October 11, 2024

WANANCHI 10,378 WAFIKIWA NA HUDUMA YA AFYA YA MACHO LINDI.





NA HADIJA OMARY, LINDI.


Jumla ya Wananchi 10,378 kutoka halmashauri sita za Mkoa wa  Lindi  wamefikiwa na huduma ya Afya ya macho ambapo kati yao 9690 wamefanyiwa vipimo na kupatiwa matibabu 



Hayo yameelezwa na Dokta Sharifu Hamza kwa niaba ya Mganga Mfawidi wa hospital ya Rufaa MKoa wa Lindi Sokoine, Jana oktoba 10 wakati wa maadhimisho ya Afya ya macho yaliyofanyika kimkoa Katika hospital hiyo ya Rufaa Sokoine huko Manispaa ya Lindi .



Zoezi hilo la utoaji Elimu ya Afya ya macho sambamba na vipimo na matibabu limeendeshwa kwa ufadhili wa mashirika ya  Heart to Heart foundation,  CBM pamoja na Korea church .


Amesema  zoezi hilo lililoendeshwa kwa siku saba kuanzia oktoba 4 hadi 10 wataalamu walipita katika shule mbalimbali kwa halmashauri zote sita kutoa elimu pamoja na kutoa matibabu kwa wananchi walioonekana na changamoto ya afya ya macho.


maadhimisho hayo ya Afya ya macho  yanayohimiza vijana na watoto kupenda macho yao na  kuitaka dunia kuongeza umakini katika upatikanaji wa huduma bora za macho kwa vijana, ambapo amesema kuwa ni faraja kubwa kwa mkoa huo ambapo zoezi hilo limefanyika kwa ufanisi mkubwa 


Hata hivyo Dokta Sharifu Ameeleza kuwa  huduma hiyo ya macho inaendelea kutolewa Katika hospital hiyo Hata baada ya wiki hiyo ya Afya ya macho kumalizika.


Edward Aloyce Afisa mradi kutoka shirika la  heart to heart foundation amesema shirika lao limekuwa likifanya mradi wa macho katika Mkoa wa Lindi wakilenga kupata watoto 20 wenye changamoto ya mtoto wa jicho ambao watanufaika kufanyiwa oparesheni Bure 


"Tumesukumwa kwa sababu watoto ndio wanapata changamoto kubwa katika tatizo la macho na tumefanya kwa ushirikiano pamoja na hospitali hii ya Lindi Sokoine lakini pia tutafanya na hospitali ya taifa ya muhimbili kwa kuleta madaktari bingwa baada ya watoto hao kuweza kuainishwa kutokana na changamoto zao za magonjwa ya macho"


Aidha  Aloyce alitoa wito kwa Wazazi na walezi Mkoani humo kujenga tabia ya kuwahimiza watoto kufanya uchunguzi wa changamoto ya macho katika hospitali ya sokoine ili kuweza kuwasiliana na wataalam hao wa hospitali ya muhimbili



Dokt Mwacha Machaja  Ni mtaalamu wa magonjwa ya macho Hospital ya Rufaa ya Lindi Sokoine amesema zipo sababu mbalimbali zinazopelekea matatizo ya macho ambapo miongoni kwa sababu hizo ni umri, ajali, lishe duni , maambukizi  na sababu za  kuzaliwa, 



Hata hivyo Amesema  sababu kubwa inayowafanya baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Lindi wamekuwa wakipata changamoto ya macho kutokana na kukosa lishe bora hali inayopelekea kuathirika kwa macho


" wakazi wengi wa Lindi wanaopata changamoto ya macho inatokana na kutokula vyakula vinavyolinda macho uwenda kwa kujua ama kutokujua kula mboga za majani zilizoiva sana ama pengine kutokula kabisa".



Nae Asha Matola mkazi wa Lindi amesema amefika hospitalini hapo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi baada ya kuugua macho kwa muda mrefu na kwamba imani yake atapata matibabu mazuri .


 

No comments:

Post a Comment