Thursday, October 3, 2024

BASHE AWAHAKIKISHIA WAKULIMA WA KOROSHO KUPATA BEI NZURI

 




NA HADIJA OMARY,  LINDI.

Waziri wa kilimo Hussain Bashe Amewahakikishia wakulima wa korosho kuwepo kwa bei nzuri ya zao Hilo Katika msimu wa mauzo 2024/2025 unaotarajiwa kuanza November 11 mwaka huu

Waziri Bashe ameyasema  hayo  November 02, 2024 akiwa Mkoani Lindi wakati anazungumza na Wadau wa kilimo ambapo Amesema kuwa kutokana  na mfumo rafiki unaotumika Katika uuzaji wa mazao wa Soko la Bidhaa (TMX) Hana Shaka kuwepo kwa bei zinazoridhisha Katika minada

" Tunaamini mwaka huu bei za korosho zitakuwa nzuri na kwa mara ya kwanza kwenye mfumo huu wa TMX tumeona makampuni ya kigeni ambayo yamejaribu kununua na zimepokea mzigo kama walivyotaka"

''Yaan wameshiriki wameiona katalog wameomba na kununua wakiwa huko huko nje na wameweza kupokea sasa maana yake   hamu imekuwa kubwa wanaweza kuuamini mfumo"

Hata hivyo Bashe ameviagiza Vyama vikuu vya ushirika Mkoa wa Lindi kufanya utambuzi wa maghara ya kuhifadhia korosho kabla ya msimu mpya wa mauzo ya zao Hilo kuanza rasm ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa korosho kwenye maghala 


"Nimewaagiza jukumu la usimamizi na uendeshaji wa maghala ni lakwao kwa sababu katalogi inatengenezwa na chama cha ushirika , sasa kama unatengeneza katalogi kwa nini kesho unapotokea upungufu Mimi siusiki?"

Amesema ili uingie mzigo hewa Katika ghala ni lazima uanzie kwenye chama cha msingi AMCOS ili kupata uthubitisho kutoka chama kikuu cha ushirika na mwendesha ghala hivyo ili kukabiliana na Hilo lazima vyamavikuu vikasimamia na endapo kutatokea udangajifu  wa Aina yoyote na wao watahusika 

No comments:

Post a Comment