Tuesday, October 8, 2024

DC MWANZIVA NSSF: LINDI ONGEZENI KUTOA ELIMU KWA WANACHI UMUHIMU WA KUJIUNGA NA MFUKO NA FAIDA ZAKE

 





Na Hadija Omary, LINDI.


MKUU wa Wilaya ya Lindi Mkoani Humo Bi.Victoria Mwanziva  amewataka watumishi WA Mfuko wa hifazadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Lindi kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi wengi juu ya Umuhimu wa kujiunga na mfuko huo na faida zake


Mwanziva ametoa Rai hiyo oktoba 07/2024 wakati akizungumza na watumishi na wanachama wa Mfuko huo wa NSSF Mkoa wa Lindi Katika uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja uliofanyika huko manispaa ya Lindi .


Mwanziva Amesema wakati huu ambao Mfuko umeboresha mfumo wa sekta isiyo rasmi kwa wanachama waliojiajiri na kuandaa skimu maalumu kwa wafanyakazi walio Katika sekta rasmi ili kuweza kuchangia kwa hiari kupitia skimu hiyo ya (NISS NA SS)  pamoja na mambo mengine zinalenga kupanua wigo wa huduma za hifadhi ya Jamii hivyo ni wajibu wao kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi .


Mifuko hii ya Watu kujichangia wenyewe ebu twendeni tukaongeze Elimu kwani tuna wananchi wengi Sana ambao wamejiajiri wafanyabiashara, wajasiriamali tuweke mpango kabambe Katika wiki hii ya huduma kwa wateja kuwafikia wengi na kuwaelimisha  namna ya kujichangia na faida za kujichangia .


Kwa kutumia wiki hii ya huduma kwa wateja wanaweza kuwavutia wananchi wengi ambao huwenda mpaka sasa bado hawafahamu faida za mifuko hii ya hifadhi ya Jamii kuanza kuchangia kwa  hiari .



Katika hatua nyingine Mwanziva pia aliwakumbusha wanachama  kuhakiki taarifa za michango wanapokuwa kazini ili kuepuka usumbufu wa kufuatilia michango wanapokuwa tayari kustaafu au nje ya ajira .


Kwa upande wake meneja wa NSSF Mkoa wa Lindi Juma Namuna Amesema Mfuko umekuwa unaweka mikakati ya kuongeza uandikishaji mwaka Hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2023/2024 Mfuko huo uliweza kuandikisha wanachama wapya 291,266 huku mwaka 2024/2025 ukilenga kuandikisha wanachama wapya 324,321.


"Lakini pia kwa upande wa ukusanyaji wa michango tulikuwa tunalengo la kukusanya  Bilioni mbili Milioni miatisa na sitini na tatu  na tuliweza kukusanya Bilioni mbili milioni miatano na themanini na  saba sawasawa na ufanisi wa asilimia 87.30%"


Baadhi ya wanachama wa Mfuko huo wamesifu huduma wanazozipata kutoka Katika Mfuko na kuwasihi wananchi wenzao kujiunga ili waweze kupata manufaa.


No comments:

Post a Comment