Friday, December 23, 2016

MTOT MCHANGA ATUPWA MSIKITINI KIWANGWA WILAYANI BAGAMOYO.

Mtoto mchanga ameokotwa ndani ya Msikiti wa Kiwangwa Wilayani Bagamoyo ambae ametupwa na mtu asiyejulikana.

Kwa mujibu wa Taarifa kutoka msikitini hapo zinasema kuwa mtoto huyo aliachwa msikitini hapo  mara baada ya kumalizika  kwa swala ya ijumaa.

Kwa muji bu wa viongozi wa msikiti huo, mtoto huyo aligundulika mara baada ya kumalizika swala na watu wote kutawanyika msikitini hapo upan de wa kinamama.

Aidha, pem beni ya mtoto huyo kumeachwa kadi ya Kliniki ambayo haijaandikwa kitu chochote pamoja na  barua yenye maelezo haya   

"ASALAMU  ALAYKUM WARAHMATULLAAHI,  WABARAKATUH, NDUGU ZANGU WAISLAMU, MIMI NILIYEMUWEKA HAPA MTOTO SI MZAZI WA MTOTO HUYU, BALI NIMEKABIDHIWA NA BINTI KWENYE GARI, KANIAGA ANAENDA KUJISAIDIA HAKURUDI TENA, NIMEANGALIA KWENYE MFUKO WAKE NIKAKUTA BARUA INASEMA huyo mtoto ni wako, KWAKUWA MIMI BADO NI MSAFIRI SITOMUWEZA, KWAHIYO NAOM BA MSIKITINI WA KIWANGWA MUMPOKEE HUYU ALELEWE KATIKA  MAADILI YALIYOKUWA MEMA, BASI YEYOTE  ATAKAJITOLEA KUMLEA MTOTO HUYO ATAKUWA WAKWAKE, KWANI MTOTO HANA DHAMBI,  ASALAAMU ALAYKUM." 
mwisho wa kunukuu.
Mtoto huyo ameokotwa kwenye Msikiti wa Suna waljamaa ambaounamilikiwa naTaasisi ya SirajulMunir Islamic Center yenye makao yake makuu mjini Bagamoyo.

No comments:

Post a Comment