Friday, December 2, 2016

WANANCHI WAZUIA MSAFARA WA MBUNGE WA JIMBO. LA MKURANGA ABDALLAH ULEGA

ule2
Mbunge wa  Jimbo la Mkuranga Mkoani Pwani, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kibuyuni  Kata Panzuo baada kufunga barabara kwa lengo la kufikisha malalamiko yao.
 ule3
Mkazi wa kijiji cha Kibuyuni  Kata Panzuo,Juma Mwengele akizungumza kwaniaba ya wananchi wezake  wa Kata ya Panzuo juu ya Ng’ombe ambao wanapita kuharibu vyanzo vya Maji na hata mazao.
 ule4
Mbunge wa  Jimbo la Mkuranga ,Abdallah Ulega akikagua timu kabla ya mchezo wa Kombe la Ulega Cup.
...........................
 
WANANCHI wa Kata ya Panzuo wamelazimika kufunga barabara kwa lengo la kufikisha malalamiko yao Kwa  Mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega ambaye Alikuwa anatoka kijiji cha mkuruwili, kusikiliza kero yao hususani Ng’ombe ambao wamekuwa tatizo kubwa katika Wilaya ya Mkuranga.

Wananchi hao ambao walilazimika kukaa katikati ya barabara walimweleza Mbunge Ulega kwamba wanataka kusikia kauli yake juu ya uharibufu unaofanywa na Ng’ombe hao.
 
Akizungumza kwaniaba ya wananchi wezake  Mkazi wa kijiji hicho Juma Mwengele alisema kuwa wamelazimika kufunga barabara ili kuonesha hisia zao kwamba wanakerwa na uharibufu unaofanywa na Ng’ombe ambao wanapita kuharibu vyanzo vya Maji na hata mazao.
 
“Ndugu mbunge kwaza tunaomba samahani sana Kwa kuharibu utaratibu wako lakini tumeladhimika kufanya hivyo kutokana na wanyama wanaitwa ng’ombe,kwakweli wanatuasili mno na tuseme tu hatuwataki sisi.”alisema Mwengele.
 
Aliongeza kuwa ng’ombe wamekuwa tatizo kubwa na kadri siku zinavyokwenda hali inazidi kuwa mbaya mno kwani wanyama hao kila siku wanaingia Kwenye maeneo muhimu hususani kwenye vyanzo vya Maji pamoja na mashambani.

No comments:

Post a Comment